Skip to main content

Ubaguzi wa Kijinsia, wasababisha wanafunzi wakike kutokushiri baadhi ya michezo.

Na, Hassan Msellem, Pemba 


Suala la ubaguzi wa Kijinsia kwenye michezo maskulini ni moja miongoni mwa sababu zinazopelekea wanafunzi wakike kutoshirikishwa kwenye baadhi ya michezo ikiwemo mpira wa miguu.


Hayo yamedhihirishwa na wanafunzi wakike na walimu kwenye Skuli mbali mbali Kisiwani Pemba, wakati mwandishi wa Habari hizi alipofanya mahojiano na walimu na wanafunzi juu ya suala la usawa wa Kijinsia kwenye michezo maskulini.


Hajra Jabir Suleiman na Nadra Juma Rajab ni wanafunzi wa Skuli ya msingi Michakaini Chake Chake Chake Pemba ambao wanashiriki michezo mbali mbali skulini hapo wamelalamikia suala la kubaguliwa kwenye michezo kama vile mpira wa miguu kwa kisingizio cha jinsi yao ya kike huku mchezo huo ukinasibishwa na Vijana wakiume pekee.


"Licha ya kucheza Netball na Nage lakini napenda kucheza mpira wa miguu pia ila kila ninapomuambia Mwalimu wa michezo ananikatalia anasema wanawake haturuhusiwi kucheza mpira" alisema Hajra


"Mwanzo nilikuwa napenda kuangalia wanaume wakicheza mpira nami nikavitiwa na kucheza mpira lakini nilipomuambia mwalimu akasema uwanjani nitakuwa mwanamke peke yangu itakuwa sio vizuri" Nadra Juma Rajab 

Habiba Juma Jafar ni mwalimu wa somo la michezo Skuli ya msingi Michakaini, alisema kutokuwepo kwa mazingira mazuri ya kimichezo katika skuli hiyo ni moja miongoni mwa sababu zinazowakosesha nafasi wanafunzi wa kike kushiriki kwenye baadhi ya michezo ikiwemo mpira wa miguu.


"Sio kwamba tunawakataza wanafunzi wakike kushiriki katika michezo wanayocheza wanaume ikiwemo mpira wa miguu lakini ukiangalia kwanza wanafunzi wenyewe wakike sio wengi wanaopenda kucheza mpira lakini hata hao wachache waliopo tuna shida ya eneo la kuchezea maana ukiangalia tulikuwa na Uwanja lakini eneo Hilo kwasasa linajengwa na Skuli yetu Haina eneo kubwa la wazi, lakini hata baadhi ya walimu hawako tayari kuwaruhusu wanafunzi wakike kushiriki kucheza mpira kutokana na Mila na desturi zetu" alisema

Afisa michezo wa Skuli za msingi Wilaya Chake Chake Abass Daud Juma, alisema sera ya michezo kwenye sekta ya elimu ya mwaka 2018 imeweka usawa wa Kijinsia kwenye suala michezo maskulini sambamba na mazingira wezeshi kwa watu wenye mahitaji maalumu ili kuwepo kwa usawa kwenye sekta hiyo, ingawa sera hiyo bado inaendelea kukumbana na changamoto mbali mbali ikiwemo ukosefu wa viwanja vya kufanyia mazoezi.


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...