Skip to main content

Kijana wa Miaka 20 agongwa na Gari akiwa anaendesha Vespa na kufariki Dunia.

 Na, Hassan Msellem, Pemba


Kijana Mbarouk Salum Mbarouk 20, Mkaazi wa Kipapo Shehia ya Chonga Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki baada ya kupata Ajali ya kugongwa na Gari akiwa anaendesha chombo Cha maringi mawili aina ya Vespa katika Eneo la Kipapo Pemba.

Tukio Hilo limetokea March 24 Majira ya saa 7 za Mchana Huko katika Eneo la Kipapo Shehia ya Chonga Mkoa wa Kusini Pemba.

Akikiri kupokea mwili wa Marehemu huyo Daktari Dhamana wa Hospital ya Chake Chake Abraham Said Msellem, amesema March 24 Majira ya saa 8:30 za Mchana amepokea Kijana anaekadiriwa kuwa na Miaka 20 ambaye alipata Ajali ya kugongwa na Gari na kuumia maeneo mbali mbali ya mwili wake ikiwemo mbele ya fuvu la kichwa mkono wa kulia.

Aidha amesema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa Marehemu alipata majeraha makubwa katika Eneo la fuvu la kichwa jambo ambalo lilisababisha kuvuja Kwa damu na kupotezea Maisha punde wakati akifanyiwa matibabu.

Ili kupata ufafanuzi juu ya ajali hiyo Mwandishi wa Habari hizi alimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba lakini jitahada za kumpata ziligonga mwamba.

Ajali za Barabarani ni Moja miongoni mwa matukio yanayotokea mara Kwa mara Visiwani Zanzibar huku Chanzo Cha Ajali hizo kikitajwa kuwa ni Mwendo Kasi, ulevi pamoja kutokuzingatia Sheria za Usalama Barabarani.

Kifo cha kijana huyo kimefikisha idadi ya watu nane kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi January 2022, katika Mkoa wa Kusini Pemba.


Habari hii niliichapisha kwenye ukurasa wangu wa Facebook March 26, 2022 kwa ushahidi wa kiungo (link) hichi kabla ya kuanzisha blog ya Pemba Post ambayo nimeichapisha habari.

Link of Facebook above👇

https://www.facebook.com/share/p/zPTMPzMppcbAfbUX/?mibextid=oFDknk

Mwisho.


Story By English.

And, Hassan Msellem, Pemba



Kijana Mbarouk Salum Mbarouk 20, Resident of Kipapo Shehia Ya Chonga District Chake Chake South Pemba Region, has died after being hit by a car while driving a Vespa in Kipapo Pemba.

The event happened on March 24 around 7 o'clock in the afternoon in the area of Kipapo Shehia of Chonga, South Pemba Region.

Acknowledging that he received the body of the deceased, Doctor Dhamana of Chake Chake Hospital, Abraham Said Msellem, said that on March 24, around 8:30 in the afternoon, he received a young man estimated to be 20 years old who had an accident when he was hit by a car and injured various parts of his body. including the front of the skull on the right hand.

In addition, he has said that the preliminary examination shows that the Deceased suffered serious injuries in the area of the skull which caused bleeding and lost his life soon while undergoing treatment.

In order to get an explanation about the accident, the reporter of this news looked for the South Pemba Regional Police Commander, but efforts to find him were unsuccessful.

Road accidents are one of the events that occur regularly in the Zanzibar islands, with the cause of these accidents being speeding, drunkenness, and disregarding Road Safety Laws.

The death of the young man has reached eight people in a period of three months from January 2022, in the South Pemba Region.

The End.
All reacti

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...