Na, Thuwaiba Habibu.
Muanzilishi wa kike vikundi vya ushirika kutoka mkoa wa kusini bi lela Hamadi Makame amewataka wanawake kugombea nafasi za uongozi kwani wao ndio watatuzi wakubwa wa shida za wanawake wenzao.
Ameyasema hayo wakati akitoa mafunzo katika kikundi cha ushirika kiitwacho "hizo ndio fikra zenu"huko koani wilaya ya kati mkoa wa kusuni unguja amesema kuna wanawake wanakabiliwa na matatizo mengi ndani ya jamii yetu na wanashindwa pakuyapeleka na kubakia yakiwathiri wao na vizazi vyao.
Alisema kabla ya kuwa kuanzisha vikundi hivi na kupata nafasi hii ya uongozi nilikuwa mama wa nyumbani tu lakini kitu kilicho nisukuma ni kuona wanawake wanadhalilika hasa wale ambao wameachwa na waume zao na kufikia hatua ya ya kutumia miili yao ili waweze kukidhi haja zao na watoto wake.
"Inafika wakati mwanamke anachuma mali na mume wake lakini wakiachana anamfukuza na kumuachia watoto ambao hajuwi hata awapeleke wapi"
Aidha alisema hakuna mwanamke hata mmoja ambaye hawazi kuongoza, kitu cha msingi ni kuondoa hofu na kugombania nafasi hizo kwani wao ndio wawakilishi wazuri kwa wenzao.
Vile vile alisema utayari unahitajika kwa jambo hilo na utawafanya waweze kufika katika sehemu wanayoitaka kwani walishaweza kuongeza familia hilo zoezi tosha la kumudu uongozi.
Nae mwanachama wa kikundi hicho amesema kwasasa wanawake wanatakiwa wapatiwe elimu zaidi juu ya suala la kuwa viongozi kwani wanao uwezonwa kujikomboa wao wenyewe bila ya kusubiri nguvu kutoka kwa mwanamme.
Na sheha wa koani bi tunza Ali shaali amesema yeye ni kiongozi wa kwanza kuwa sheha wa kike kwa Zanzibar na ameweza kuongoza kijiji hicho hali ya kuwa wanaume walikuwa ni wengi katika uongozi na akafanikiwa bs kila mwanamke anao uwezo huo jambo muhimu ni utayari wa suali hilo

Comments
Post a Comment