Skip to main content

Wanaume wajitoa kuhakikisha wanawake wanakuwa juu kiuchumi na uongozi.

Na, Thuwaiba Habibu.

Mwalimu wa vikundi vya kueka na kukopa kutoka Umbuji kheri Omari amewataka wanawake kutumia vikundi kujifunza uongozi pamoja na kujikwamua kiuchumi.


Amesema hayo wakati akizungumza na muandishi wa habari hizi huko umbuji wilaya ya kati mkoa wa kusini unguja amesema ndani ya vikundi ni rahisi kwa wanawake kuweza kujifunza uongozi kwasababu vikundi ni wanawake watupu na kuna nafasi mbali mbali za kuwajengea uzoefu.


"kuna nafasi za mwenyekiti , makatibu na washika hazina hivyo basi nafasi hizi wakizitekeleza kiuwadilifu ikitokea nafasi ya uongozi wa juu inakuwa ni wepesi kwa mtu kugombea na kutekeleza majukumu yao kiusahihi.


Pia alisema najitahidi kuwamasisha wanawake kuwa imara katika shughuli za vikundi na uongozi kwani watajikwamua kiuchumi na kuleta maendeleo katika nchi zetu.


Huu sio muda tena wa mwanamke kusubiri kulitewa na kuongozwa tu bali wanawake watakiwa wapambane kutafuta ila kwa utaratibu mzuri.


Kwa upande wake katibu wa kikundi cha wanawake na maendeleo khadija fundi hiari alisema mwalimu kheri ni mtu ambaye yupo na mawazo hali juu ya wanawake kuongoza na kuweza kumiliki Mali zao kitendo hicho kilimfanya azishe kikundi kwani ingekuwa vigumu kupita kila nyumba kuhamasisha.


Vile vile alisema mwalimu huyo ni kigezo cha kuigwa na wanaume wote kwani kupoteza muda wake kwa ajili ya wanawake hilo ni suala la ujasiri sababu wanaume wengi hushindwa kufanya jambo hilo.


Nae mwanakikundi mwengine bi chiku ramadhani anaeleza kuwa kama watajikokeza wanaume wengine kama bwana kheri Omar kuwaunganisha wanawake kwa kuwaanzishia vikundi basi itakuwa ni kitu Cha muhimu na wanawake watajiimarisha kiuchumi na watajifunza zaidi kuongozi na watakuwa sio tegemezi Tena kwani watakuwa na muamko wa kimaendeleo.


Pia alisema tunataka kufanye kazi kwa kuendana na kauli mbiu ya mama Samia ya hapa kazi tu kauli hii itazidi kuwahamasisha kushiriki kikamilifu katika masuala ya uongozi.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...