Habari Na, Nihifadhi Issa
Zanzibar.
Mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA Zanzibar Dkt. Mzuri Issa amesema Sheria nambari 5 ya wakala wa habari, magazeti na vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho sheria namba 8 mwaka 1997 sheria hii licha yakuwa ni kongwe imekuwa na mapungufu mengi yanayokwamisha haki na uhuru wa vyombo vya habari Zanzibar.
Akizungumza katika kikao cha kujadili mapungufu ya sheria zinazokwamisha uhuru wa habari huko katika ukumbi wa TAMWA Tunguu amesema Demokrasia sahihi hutegemea uhuru wa vyombo vya habari unavyoweza kusimamia maslahi ya jamii, ikiwemo uhuru wa kutoa maoni na kujieleza bila ya kuingiliwa pamoja kusambaza taarifa na mawazo ya aina mbalimbali kwa kufuata kanuni zilizowekwa ni haki inayotambuliwa na sheria za kitaifa na kimataifa.
“ikiwa Zanzibar imo ndani ya Tanzania na imeridhia mikataba mbalimbali ambayo inalinda tasnia ya habari ipo haja kufanyika marekebisho kwa sheria ambazo haziendi sambamba na uhuru wa habari ikiwemo sheria hii” alisema
Dkt MzuriKwa mujibu wa Sheria nambari 5 ya wakala wa habari, magazeti na vitabu ya mwaka 1988, yenye marekebisho ya sheria namba 8 mwaka 1997 katika sheria hii vipo vifungu ambavyo havijatowa uhuru kwa waandishi pia kwa vyombo vya habari kikwemo kifungu cha 14 (1) kilichompa mamlaka mrajisi kumtaka mchapishaji gazeti kupeleka kopi mbili kila siku kwa gharama zake kwa madai ya kuweka kumbukumbu.
Afisa mratibu boresha habari kutoka chama cha waandishi wa habari wanawake tamwa-zanzibar kwa kishirikiana na internews tanzania Zaina Abdalla Mzee uwepo wa sheria hiyo unakinza dhana ya demokrasia na utawala.
“kwanza hii sheria ni kongwe imefikia wakati irekebishwe ili kuchapuza uhuru wa habari ambao tunautaka”
Waandishi wa habari ndio wahusika wakuu katika hili, Khatib Suleiman ni mwandishi wa habari wa gazeti la Habari Leo anasema vifungu hivyo vya sheria vinarudisha nyuma utendaji wa kazi wa mwandishi wa habari
“kwa mfano chombo cha habari hakipati mapato kinapata wapi fedha za kupeleka nakala kila siku kupeleka kwa mrajis mimi mawazo yangu ofisi ya mrajis iwe na mtu maalum wa kufuatilia izo habari kama wanataka kuendelea na hiyo sheria” amesema Khatib.
Wananchi wanayo haki ya kupata habari kupitia vyombo mbalimbali Mfaume muhammed anasema ikiwa vyombo vya habari vitaekewa vikwazo au vizuizi ambavyo si vya lazima itawia vigumu kupata habari
“lazima vikwazo vingine vitatuliwe ambavyo vinaonekana havina ulazima sana izo nakala mbili ni nyingi wakishindwa kuchapisha na siis wasomaji wa magezeti tutakosa kusoma habari” alifafanua mfaume

Comments
Post a Comment