Skip to main content

MAREKEBISHO YA SHERIA YA HABARI ITAKUWA CHACHU YA MAENDELEO ZANZIBAR.

 ZANZIBAR.

Na Nafda Hindi.

Mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari Tanzania TAMWA ZNZ Dk Mzuri Issa amesema kuwepo kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini kutarahisisha maendeleo ya haraka kwa Taifa.

Dk Mzuri ameyasema hayo katika mkutano wa kujadili mapungufu ya sheria zinazokwamisha uhuru wa habari Zanzibar uliwashirikisha watendaji kutoka Wizara ya Habari.Utamaduni,Utalii na Vijana, Tume ya kurekebisha Sheria Zanzibar, Tume ya Utangazaji, Kamati ya vyombo vya Habari Zanzibar (ZAMECO) na waandishi wahabari uliofanyika Ofisis za TAMWA Tunguu Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.

Akitolea mfano wa  nchi zilizopiga hatua kimaendeleo kama Marekani na kwa Afrika  ni pamoja na Afrika ya Kusini na Mozambik kwa kuvitumia vyema vyombo vya habari vimesababisha kuinua uchumi wa  nchi hizo na kuleta mabadiliko.

“Nchi yetu ina Amani na maendeleo ya kiuchumi lakini suala la uhuru wa habari ni jambo muhimu na tuna wajibu sisi wadau kuhakikisha unafikiwa na kutelelezwa ipasavyo, Dk Mzuri Issa.

Aidha amesema  pamoja na kuridhia Mikataba ya Kimataifa na Kikanda bado Tanzania sauti za wananchi hazipewi kipau mbele kusikika katika vyombo vya habari ukilinganisha na sauti za Viongozi jambo ambalo linawanyima wananchi haki yao ya kikatiba ya kutoa maoni yao.

“ Sheria, Kanuni na Sera ndizo zinazotowa mustakabal mzuri watu kuripoti habari endapo tutakuwa na sheria zisizo rafiki habari itakuwa ni ngumu kuripotika na kusababisha kukosa kasi ya maendeleo, Dk Mzuri Issa. 

Mapema Afisa mradi wa Uhuru wa Habari kutoka TAMWA ZNZ Zaina Mzee amesema sauti za wananchi zipewe nafasi ya kusikika kupitia vyombo vya habari kwa lengo la kupata maendeleo  nchini.

Akiwasilisha mada inayohusu Mapungufu ya  Sheria ya habari Mwandishi mwandamizi Hawra Shamte amesema ingawa kuna sheria zinazosimamia sekta ya habari bado zinaonekana kiuhalisia hazifanyi kazi ipasavyo kwa kulinda Usalama wa waandishi wa habari na wananchi hivyo zinahitaji kufanyiwa marekebisho.

“Mikataba mbali mbali ya Kikanda na Kimataifa inalinda tasnia ya habari, waandishi wahabari na watetezi wa haki za binadamu na kulinda wajibu wa Serikali kufuata, kuendeleza uhuru wa kutoa maoni na kujieleza, Hawra Shamte.

Mikataba hiyo ni pamoja na Tamko la Kimataifa la haki za binadamu (Universal Diclaration) na mkataba wa Haki za Kiraia na Kisiasa (ICCR) ambayo Tanzania ni moja ya nchi iliyoridhia mikataba hiyo, ambapo nchi mia moja na sabiini na mbili (172) zimeridhia mkataba wa haki za kiraia na kisiasa.

Mkataba mwengine ni mkataba wa  Bara la Afrika unaojuilikana kama mkataba wa haki za binadamu na haki za watu wa Umoja wa Afrika, uliopitishwa mwaka 1981 (Afrika Charter on Human  Peoples Right) ulianza kutumika (1986) na  mkataba huo hadi kufikia mwaka (2002) tayari ulisainiwa na nchi mia moja hamsini na tatu (153) za Afrika.    

 Bi Hawra akizitaja sheria hizo amesema ni pamoja na Sheria  ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu no 5 ya mwaka 1988 iliyofanyiwa marekebisho na sheria no 8 ya mwaka 1997 na Sheria ya Tume ya Utangazaji Zanzibar no 7 (1997) iliyofanyiwa marekebisho na sheria no 1 (2010).

Afisa Sheria kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo  Mwanaid Juma Suleiman amesema Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu no 5 (1988) iliyofanyiwa marekebisho na Sheria no 8 (1997) kwa vile mchakato wake ni wa muda mrefu tayari imeshapita katika maoni ya wadau na sasa  ipo katika hatua ya makatibu wakuu kufanyiwa marekebisho mbali mbali.

Afisa huyo amesema kwa upande wa Sheria ya Tume ya Utangazaji Zanzibar no 7 (1997) iliyofanyiwa marekebisho  na sheria no 1 (2010) Wizara husika haijapokea Sheria hiyo na kwa sasa Tume ya Utangazaji Zanzibar ndio inayoshughulikia sheria hiyo.

 Sheria hiyo ilisitishwa kuendelea na mchakato wake kwa sababu kanuni na sheria zilikuwa tofauti na inabidi hadi kufanyiwa marekebisho ziendane, na mpaka sasa hivi  Wizara haijapokea sheria hiyo,ila itakapokuja basi tutashughulika nayo haraka iwezekanavyo, Afisa sheria Wizara ya Habari, Utamaduni,Utalii na Michezo.

Nae Mwanasheria kutoka Tume ya kurekebisha Sheria Zanzibar Sabra Mahmoud Iddi amesema wanategemea mchakato wa Sheria ya habari utafanyiwa marekebisho ili kupata sheria bora zinazozingatia maslahi ya waandishi na uhuru wa vyombo vya habari.

“ Marekebisho ya sheria ni mchakato  wa muda mreu unaopitia ngazi hadi ngazi ili kupata sheria bora, hivyo amewaomba waandishi pamoja na wananchi kuwa na subra kwa lengo la kupata sheria bora zinazokwenda na wakati. Mwanasheria, Tume ya kurekebisha Sheria. 

Salim Said Salim ni mwandishi mkongwe amesema Zanzibar waandishi wanakutana na vikwazo mbali mbali wanapokuwa katika kutekeleza majukumu yao na hata vyombo vya habari hufikia hatua ya kufungiwa kutokuendelea na kazi zao za utangazaji.

Matukio kama haya Zanzibar yako mengi kufungiwa ovyo kwa vyombo vya habari na hata waandishi wanaekewa vikwazo ikiwemo kunyanganywa vitambulisho vyao vya kufanyia kazi hatua hii inawanyima wananchi kupata habari, Salim Said Salim.

Jabir Idrisa  mwandishi wahabari amesema Enzi za utawala wa Kisultan Zanzibar kulikuwa na magazeti Zaidi ya 50 ukilinganisha na hali iliopo sasa kuna gazeti moja pekee linalomilikiwa na Serikali hivyo marekebisho ya sheria yanahitajika ili kutoa nafasi kwa raia kumiliki magazeti binafsi.

Nao waandishi wahabari wamesema wanakutana na vikwazo kadhaa katika kufanikisha majukumu yao na kutowajibika ipasavyo kwa kuhofia usalama wao wakati hakuna sheria yoyote inayowalinda endapo watapatwa na tatizo.

MWISHO


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...