Katibu wa Siasa Itikadi na Uenezi Kijitoupele awaasa Vijana wa kike kugombea nafasi za ngazi ya juu ya Uongozi.
Na, Thuwaiba habibu
Katibu wa Siasa Itikadi na Uenezi katika Wadi ya Kijitoupele, Riziki Abdallah Ali, ambaye alikuwa Spika mstaafu wa Bunge wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu Cha Zanzibar (ZU) aliwaasa vijna wa kike kuacha fikra potofu linapokuja suala na kuomba nafasi za ngazi ya juu ya uongozi.
Ameyasema hayo wakati akiwa na wanachama wenzake huko katika wadi ya kijitoupele amesema bado vijana wana fikra potofu ya kuwa uongozi wa ngazi ya juu ni wa watu wazima tu na wao bado wanashikilia nafasi ndogo za ndani ya matawi hali ya kuwa uwezo wa kushika nyadhifa kubwa wanao.
Alisema vijana wengi wapo na mtazamo kuwa hawaruhusiwi kugombea nafasi ndani ya chama kwani wanajuwa wameshawekewa Umoja wa vijana (UVCCM) jambo ambalo sio sahihi.
Aidha alisema kuna hitajika elimu kwa vijana katika sehemu tofatuti kuachana na mitazamo isiyofaa na kuanza kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kugombea nafasi tofauti.
Sambamba na hayo alisema wanashukuru kuona japo hakuna wingi wa vijana wa kike waliojitokeza kugombea nafasi kubwa katika siasa ila wapo ambao wamesubutu kuonesha kuwa jambo hilo linawezekana endapo watalipa kipaombele.
Nae katibu wa Uvccm wa tawi la kwarara Abuu salehe abuu amesema wanajitahidi kutoa nafasi mbali mbali ndani ya majimbo na hata wadi kwa vijana wa kike ili kuwapa hamasa ya kushika nyadhifa kubwa.
Aidha alisema kila mwanamke anatakiwa ajitadhimini na kuacha kujiweka nyuma wakati ambao fursa zimetokea kwani kutokujiamini ndio kunakowafanya wanawake kukosa nafasi za kuongoza.
Vile vile aliwataka wanawake kutokuwa waoga na kujivisha moyo wa ujasiri kwani woga hauchochei maendeleo.
Nao wanachama katika wadi hiyo walisema vikao hivyo vingefanywa kila baada ya wiki mbili katika wadi zote hasa wakati huu tuna kwenda katika mwaka wa uchanguzi kwani kufanya hivyo kutawazindua vijana na kuona umuhimu wa kugombania nafasi za hizo pia itasaidia hasa kwa wale waliokuwa na hofu kuweza kujiamini.

Comments
Post a Comment