Na Nihifadhi Issa, Zanzibar.
Taasisi ya Zaina Foundation imesema kuna umuhimu wa kutambua usalama wa mtandaoni ili kujilinda dhidi ya udhalilishaji au upotevu wa taarifa ambazo ni siri.
Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Zaituni Njovu amesema njia moja ya usalama mitandaoni ni kuepuka kuweka wazi kila taarifa ambayo ni muhimu ikiwemo umri hali ya afya na mambo ya kifamilia.
Ameyasema hayo wakati akitoa mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari na taasisi mbalimbali namna ya kuzuia changamoto za mtandao.
“Ni vyema kutumia mitandao kwa kufuata kanuni na tahadhari ili kuwa salama na kuepukana na (cyber-crime) uhalifu wa mtandaoni” alisema Zaituni.
Amesema elimu hiyo ni muhimu kwa jamii ili kuongeza ujuzi na maarifa kwa watumiai na kubaini viashiria vya uhalifu mapema.
Nao washiriki wa mafunzo hayo wameahidi kuyafanyia kazi na kuwa mabalozi kwa wengine lengo ni kuhakikisha jamii ipo salama katika matumizi ya mitandao ambayo kutokana na dunia ilivyo hayaepukiki.



Comments
Post a Comment