Habari Na, Amina Massoud, Pemba.
Wakizungumza na mwandishi wa habarri hizi baadhi wa wanajamii waliofikiwa na kupatiwa elimu ya kujitambu wamesema kabla ya kupatiwa elimu hiyo waliojiona akinamama ni watu wa kukuaa nyumbani na kutunza familia tu jambo ambalo kumbe sio sahihi.
Rukia Ramadhani anaejishughulisha na ujasiriamali sambamba na kugombea nafsi za chaguzi za ndani amesema baada kupatiwa elimu na jumuiya hiyo imeweza kubadislisha maisha yao kuanzia ngazi ya familia mapaka kuingia katika harakati za uongozi.
Nae Sada Mohammed amesema kwasasa ameweza kuingia katika harakati za uongozi kwani elimu hiyo imeweza kumsaidia kugombania nafasi ya UWT.
Riziki Mohammed Makame ni mkurugenzi wa jumuiya hiyo amesema lengo kuu la kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ni kuwajengea uwezo wanawake na watoto wa Pemba ili kujua haki zao za msingi katika maendeleo ya kielimu kisiwani humo.
Amesema lengo hilo limekuja baada ya kuona jamii ya kisiwa cha pemba inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia kwa wanwake na watoto wanawake kutokujua haki zao za kidemokrasia pamoja na kutatua kero zinazowakabili watoto.
Kwa upande wake mratibu wa jumuiya zisizo za serikali ofisi ndogo Pemba Ashrak Hamad Ali amesema jumuiya ya JUKWAP ni jumuiya ya kupigiwa mfano katika kutetea haki za wanawake na watoto kisiwani humo.
Jumuiya ya jukwap iliyosajiliwa kupitia sharia no 6ya mwaka 1995 sheria ya usajili wa jjumuiya zisizo za kiserikali ipo ndani ya Wilaya ya mkoani Mkoa wa kusini pemba na kwa mujibu wa sense ya watu na makazi ya mwaka 2022 Wilaay hiyo inajumla ya wakaazi 135,052. MWISHO

Comments
Post a Comment