Skip to main content

Jumuiya ya kutetea haki za wanawake na watoto Pemba yasaidia wanawake kushiriki kwenye Uongozi.

Habari Na, Amina Massoud, Pemba.

Picha kutoka Maktaba.

WEPO wa jumuiya ya kutetea haki za wanawake na watoto Pemba imeweza kuwasaidia wanawake kujitambua na kuingia katika harakati za uongozi.

Wakizungumza na mwandishi wa habarri hizi baadhi wa wanajamii waliofikiwa na kupatiwa elimu ya kujitambu wamesema kabla ya kupatiwa elimu hiyo waliojiona akinamama ni watu wa kukuaa nyumbani na kutunza familia tu jambo ambalo kumbe sio sahihi.


Rukia Ramadhani anaejishughulisha na ujasiriamali sambamba na kugombea nafsi za chaguzi za ndani amesema baada kupatiwa elimu na jumuiya hiyo imeweza kubadislisha maisha yao kuanzia ngazi ya familia mapaka kuingia katika harakati za uongozi.


Nae Sada Mohammed amesema kwasasa ameweza kuingia katika harakati za uongozi kwani elimu hiyo imeweza kumsaidia kugombania nafasi ya UWT.


Riziki Mohammed Makame ni mkurugenzi wa jumuiya hiyo amesema lengo kuu la kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ni kuwajengea uwezo wanawake na watoto wa Pemba ili kujua haki zao za msingi katika maendeleo ya kielimu kisiwani humo.


Amesema lengo hilo limekuja baada ya kuona jamii ya kisiwa cha pemba inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia kwa wanwake na watoto wanawake kutokujua haki zao za kidemokrasia pamoja na kutatua kero zinazowakabili watoto.


Kwa upande wake mratibu wa jumuiya zisizo za serikali ofisi ndogo Pemba Ashrak Hamad Ali amesema jumuiya ya JUKWAP ni jumuiya ya kupigiwa mfano katika kutetea haki za wanawake na watoto kisiwani humo.


Jumuiya ya jukwap iliyosajiliwa kupitia sharia no 6ya mwaka 1995 sheria ya usajili wa jjumuiya zisizo za kiserikali ipo ndani ya Wilaya ya mkoani Mkoa wa kusini pemba na kwa mujibu wa sense ya watu na makazi ya mwaka 2022 Wilaay hiyo inajumla ya wakaazi 135,052. MWISHO 

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...