Skip to main content

"Waandishi zidisheni juhudi kuandika juu ya Sheria kinzani dhidi ya uhuru wa Habari" Bi. Hawra.

Imeandikwa na Hassan Msellem, Pemba.

Waandishi wa Habari wametakiwa kuzidisha juhudi katika kuandika habari na makala kuhusu Sheria za habari zinazokinzana na Uhuru wa vyombo Habari ili ziweze kufanyiwa maboresho.

Hayo yamesemwa na Mwandishi Mkongwe Visiwani Zanzibar Bi. Haula Shamte wakati akiwasilisha mada juu ya Sheria kinzani dhidi ya uhuru wa Habari katika Ofisi za Tamwa Kisiwani Pemba ambazo ni Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, magazeti na vitabu namba 5 ya mwaka 1988 iliyofanyiwa marekebisho na Sheria namba 8 ya mwaka 2010, Sheria ya Tume ya Utangazaji namba 7 ya mwaka 1997 iliyofanyiwa marekebisho na Sheria namba 1 ya mwaka 2010.

"Tukiangalia Sheria zote hizo tatu zinakinzana na falsafa ya Uhuru wa vyombo vya habari na Waandishi wa Habari kama ilivyoolezwa katika sura ya tatu ibara ya 18 ya katiba ya Zanzibar, hivyo basi ni jukumu letu wanahabari kuhakikisha tunaandika habari zaidi na makala mbali mbali Ili kuongeza ushawishi kwa vyombo vya kutunga Sheria katika kuzifanyia maboresho Sheria hizo" alisema 

Aidha amewataka Waandishi hao kuzifahamu Sheria zinazowaongoza katika utekelezaji wa majukumu yao na zile zenye mapungufu Ili waweze kuzifanyia kazi ipaswavyo.

Alisema "Fani ya habari ni kama fani nyengine inaongozwa kwa Sheria na kanuni mbali mbali hivyo munapaswa kuzifahamu Sheria na kanuni hizo sambamba na kuzitambua vyema zile Sheria na ibara zinazokwenda kinyume na uhuru wa vyombo vya habari Ili muweze kutekeleza majukumu kwa ufanisi zaidi pamoja na kuongeza uchechemuzi kwe zile Sheria ambazo sio rafiki katika muhimili wa Habari ziweze kufanyiwa maboresho"

Mwandishiwa Habari kutoka Klabu ya Waandishi wa Habari Pemba (PPC) Amina Ahmed, alisema bado Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba wanakabiliwa na changamoto kadhaa katika utekelezaji wa majukumu yao ikiwemo kupata vitisho kutoka kwa viongozi wa Serikali.

"Waandishi wa Habari Pemba kwasasa tunapitia wakati mgumu sana yani ukiandiga chochote kinachohusiana na kuiwajibisha taasisi au mamlaka fulani ghafla unapokea simu ya vitisho kutokana na habari hiyo na kutakiwa uifute haraka laa si hivyo utakutwa matatizo fulani hali hii inatunyima uhuru sana Waandishi" 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Uchechemuzi na Utatezi kutoka Tamwa Zanzibar Bi. Shifaa Said Hassan, amesema endapo Waandishi Habari watatumia kalamu zao vizuri watasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuchochea kufanyiwa maboresho Sheria hizo.

"Tumeamua kushirikiana na nyinyi Waandishi wa Habari katika kuongeza Kasi ya Uchechemuzi na Utatezi juu ya Sheria hizi kandamizi kwa vyombo vya habari na Waandishi wa Habari kwa ujumla kwa kuamini kuwa sauti zenu na kalamu zenu zinafika mbali sana na kwa haraka zaidi, hivyo basi ni wajibu wenu kuhakikisha munatumia kalamu zenu vizuri katika kuhakikisha munaandika Habari na makala mbali mbali juu ya Sheria hizi kusudi zifanyiwe maboresho" alisema Bi. Shifaa Said Hassan 

Wakitoa neno baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo Waandishi hao wameahidi kuandika habari na makala zaidi juu ya Sheria hizo zenye mapungufu kufanyiwa marekebisho Ili waweze kutekeleza majukumu kwa ufanisi.



Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...