Imeandikwa na
Hassan Msellem, Pemba
Mradi wa
Uhamasishaji wanawake kushiriki katika Uongozi (SWIL) unaoendeshwa na
taasisi tatu ambazo ni Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania
(TAMWA) Zanzibar, Jumuiya Utetezi wa Mazingira na Kijinsia Pemba (PEGAO)
pamoja na Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) kupitia
madarasa ya kisomo Shehia ya Mjini Kiuyu umefanikiwa kuongeza idadi ya akina mama wenye uwezo wa
kujua kusoma na kuandika ili waweze kushiriki vyema katika shughuli za kijamii,
kisiasa na uongozi.
Mariam Juma
Hamad ni Mwalimu wa darasa la Kisomo Shehia ya Mjini Kiuyu amesema licha ya
changamoto mbali mbali zinazolikabili darasa hilo lakini limeweza kutoa mwanga
kwa akina mama wengi kujua kusoma na kuandika ikilinganishwa na hapo awali
kabla ya kuanzishwa kwa darasa hilo.
“Kwakweli darasa
hili limetusaidia sana akina mama wa Shehia ya Mjini Kiuyu wengi walikuwa
hawajui kusoma wala kuandika hata majina yao lakini tangu kuanzishwa kwa darasa
hili takriban akina mama khamsini wana uwezo wa kusoma sehemu yoyote
iliyaondikwa lugha ya Kiswahili na wana uwezo pia wakuandika pia” alisema Bi.
Mariam mwalimu wa darasa la kisomo Shehia ya Mjini Kiuyu
Ruwaila Ali
Haji, ni miongoni mwa mwanafunzi na mnufaika wa darasa hilo la kisomo alisema darasa
hilo limemuwezesha kwa kiasi kikubwa kujua kusoma na kuandika kwani awali
hakuwa na uwezo hata wakusona na kuandika jina lake.
“Kabda ya
kujiunga na darasa hili la kisomo nilikuwa sijui kusoma wala kuandika hata jina
langu moja lakini sasa hivi nina uwezo wakusoma maandishi yoyote ya lugha ya kiswahili
pamoja na kuandika jambo ambalo lisingekuwa rahisi kwangu kama kusingekuwa na
darasa hili la kisomo” alisema
Inaendelea…………….


Comments
Post a Comment