Skip to main content

Mradi wa "SWIL" wawezesha akina Mama zaidi ya 50 kujua kusoma na kuandika Shehia ya Mjini Kiuyu.

Imeandikwa na Hassan Msellem, Pemba 

Mradi wa Uhamasishaji wanawake kushiriki katika Uongozi (SWIL) unaoendeshwa na taasisi tatu ambazo ni Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania (TAMWA) Zanzibar, Jumuiya Utetezi wa Mazingira na Kijinsia Pemba (PEGAO) pamoja na Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) kupitia madarasa ya kisomo Shehia ya Mjini Kiuyu umefanikiwa kuongeza idadi ya akina mama wenye uwezo wa kujua kusoma na kuandika ili waweze kushiriki vyema katika shughuli za kijamii, kisiasa na uongozi.

Mariam Juma Hamad ni Mwalimu wa darasa la Kisomo Shehia ya Mjini Kiuyu amesema licha ya changamoto mbali mbali zinazolikabili darasa hilo lakini limeweza kutoa mwanga kwa akina mama wengi kujua kusoma na kuandika ikilinganishwa na hapo awali kabla ya kuanzishwa kwa darasa hilo.

“Kwakweli darasa hili limetusaidia sana akina mama wa Shehia ya Mjini Kiuyu wengi walikuwa hawajui kusoma wala kuandika hata majina yao lakini tangu kuanzishwa kwa darasa hili takriban akina mama khamsini wana uwezo wa kusoma sehemu yoyote iliyaondikwa lugha ya Kiswahili na wana uwezo pia wakuandika pia” alisema Bi. Mariam mwalimu wa darasa la kisomo Shehia ya Mjini Kiuyu


Mariam Juma Hamad, Mwalimu wa darasa la Kisomo Shehia ya Mjini Kiuyu.

Ruwaila Ali Haji, ni miongoni mwa mwanafunzi na mnufaika wa darasa hilo la kisomo alisema darasa hilo limemuwezesha kwa kiasi kikubwa kujua kusoma na kuandika kwani awali hakuwa na uwezo hata wakusona na kuandika jina lake.

“Kabda ya kujiunga na darasa hili la kisomo nilikuwa sijui kusoma wala kuandika hata jina langu moja lakini sasa hivi nina uwezo wakusoma maandishi yoyote ya lugha ya kiswahili pamoja na kuandika jambo ambalo lisingekuwa rahisi kwangu kama kusingekuwa na darasa hili la kisomo” alisema 

Inaendelea…………….

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...