Skip to main content

“Bado kuna pengo kubwa kwa Waandishi wa Habari kuandika Habari za mabadililo ya tabia ya Nchi na Usawa wa Kijinsi” Dr. Mzuri Issa Mkurugenzi Tamwa, Zanzibar

 Waandishi wa Habari Zanzibar wametakiwa kuongeza bidii katika kuandika Habari zinazohusu Usawa wa Kijinsia na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi ili kuleta msukumo wa mabadiliko katika jamii na Taifa.



Akizungumza na Waandishi wa Habari na wadau mbali mbali Mkutano wa Uchambuzi kwa vyombo vya Habari juu Usawa wa Kijinsia na Uongozi na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi Mkurugenzi wa Tamwa Zanzibar Dr. Mzuri Issa, amesema tafiti zinaonesha bado kuna nafasi ndogo kwa vyombo vya Habari kuandika na kuripoti Habari za Usawa wa Kijinsia na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi hali inayobabisha ufahamu mdogo wa jamii katika Nyanja hiyo.

 

“Utafiti unaonesha ushiriki wa Waandishi wa Habari kuandika Habari za usawa wa kijinsia na mabadiliko ya tabia ya nchi bado ni mdogo sana na badala yake waandishi wa Habari wanaelekeza zaidi macho yao kwenye Habari za udhalilishaji, michezo kiasi kwamba hata kwenye vyombo vyao Habari za usawa wa kijinsia na mabadiliko ya tabia ya nchi hazipewi kipaumbele” alisema

 

Akitoa mapendekezo katika mkutano huo Mkufunzi wa chuo kikuu cha Zanzibar (ZU) na Mtafiti wa Mazingira na vyombo vya Habari Salum Suleiman, amependekeza kuboreshwa kwa Sera zitakazowawezesha wanawake kupewa kipaumbele kushiriki katika shughuli za mabadiliko ya tabia ya Nchi.

 

Alisema “Tutokeni kwenye ile tafsiri kwamba vyombo vya Habari vina jukumu la kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha na badala yake tutumieni vyombo vyetu kuandika Habari zenye kuleta mabadiliko Chanya kwenye jamii zetu n ahata taifa kwa ujumla”

 

Kwa upande wake mwakilishi kutoka taasisi ya Community Forest Pemba, amesema kutokana shughuli za kibidamu ikiwemo kilimo na upigaji wa mkaa maeneo mengi ya Kisiwa cha Pemba na Unguja yameathirika kutokana na mabadiliko ya tabia ya Nchi.

 

“Kama tunavyofahamu kuwa kadri siku zinavyosonga idadi ya watu inaoongezeka na shughuli za kibinadamu zinaongezeka pia ikiwemo ujenzi nakdhalika kwahivyo kuna kila haja ya kubuni njia mbadala wa kutumia miti kwa kiasi kikubwa katika shughuli zetu za kila siku ikiwemo nishati za kupikia ili kuepukana na madhara ya mabadiliko ya tabia ya nchi ambayo kwa kiasi kikubwa yanamuathiri mwanamke” alisema

 

Nao washiriki wa Mkutano huo wamependekeza kutolewa kwa mafunzo maalumu kwa Waandishi wa Habari na Wadau wa Mazingira na Usawa wa Kijinsia ili waweze kuandika na kuripoti Habari hizo kwa ufanisi.

 

“Katika Uchambuzi wetu hapa tumeona kuwa miongoni mwa sababu zinazosababisha vyombo vya Habari kutokuandika Habari za Usawa wa Kijinsia na Mabadiliko ya tabia ya Nchi ni pamoja na kutokuwa na ujuzi wa kutosha katika Nyanja hiyo hivyo basi napendekeza kuandaliwe kwa mafunzo maalumu kwa waandishi wa Habari na wadau wengine waweze kufahamu kwa kina kuhusu usawa wa kijinsia na mabadiliko ya tabia ya Nchi ili waweze kaundika Habari hizo kwa ufanisi zaidi na ziweze kuleta tija katika jamii na taifa kwa ujumla”

                                                                                              

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...