NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Jumla ya makala 253, zinazohusu masuala ya uhuru wa habari Zanzibar zimeripotiwa na kuchapishwa kupitia magazeti, redio za kijamii na kitaifa pamoja na mitandao ya kijamii. Makala hizo zimeandikwa na waandishi wa habari 25 waliopata mafunzo maalum kutoka vyombo mbalimbali vya habari vya Unguja na Pemba. Hayo yameelezwa na Afisa Programu ya Mapitio ya sheria na uhuru wa habari kutoka TAMWA-ZNZ, Zaina Abdalla Mzee, wakati akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa programu hiyo. Katika wasilisho hilo Zaina alibainisha mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza pamoja na mikakati ya baadaye kwa ajili ya kuendeleza juhudi za kulinda na kuimarisha uhuru wa habari visiwani Zanzibar. Zaina alibainisha kuwa juhudi za ushawishi na uchechemuzi zilizofanywa na wadau wa habari, wakiwemo Wajumbe wa Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO), waandishi na wahariri habari, zimezaa matunda kwa kufanikisha kufanyika kwa mikutano mbalimbali na baadhi ya...