Skip to main content

"WAHIMIZENI AKINA BABA KWENDA KILINIKI NA WAKE ZAO KWA MASLAHI YA AFYA YA MAMA NA MTOTO" BIKOMBO ABDALLA MASTUR

Na, Hassan Msellem, Pemba 

Wafanyakazi wa afya wa jamii (CHW) na Wauguzi wametakiwa kuwahamasisha akina mama kwenda kiliniki na wenza wao ili kuimarisha afya ya mama na mtoto.

Akifunga mafunzo ya siku kwa wafanyakazi hao afya wa jamii na wauguzi huko katika ukumbi wa Baraza la Mji Wete Bikombl Abdalla Mastur, Muuguzi dhamana Wilaya ya Wete na Mratibu wa huduma za Mama, katika ufunguzi wa mradi wa miaka miwili wa Kubadilisha Mtazamo wa Majukumu ya Kijinsia na Kuimarisha Maisha ya Wanawake na Wajawazito na Wanaonyonyesha katika familia za Vijijini Pemba unaondeshwa na Jumuiya kupunguza, amesema tafiti zinaonesha bado kuna ushiriki mdogo wa akina baba kuongozana na wake zao kwenda kwenye vituo vya afya hali inayosababisha maendeleo duni ya kiafya ya mama na mtoto.

Mratibu wa Jumuiya ya kupunguza umasikini na kuboresha Maisha ya watu Pemba (PEPOHUDA) Said Mbarouk Juma, amesema lengo la mradi huo ni kutoa elimu na kuwahamasisha akina baba kushirikiana na wenzao kwenda katika vituo vya afya ili kuimarisha afya ya mama wajawazito na mtoto.

Said Rashid Hassan, Mjumbe Jumuiya Pepohuda, amewataka wahudumu hao kutanguliza uzalendo katika utekelezaji wa majukumu yao katika kutoa huduma bora kwa Wananchi.

Afisa tabibu Kituo cha Afya Jadidi Wete Fatma Amour Hemed, amesema kituo cha Afya Jadidi kinakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ukosefu wa vitendea kazi muhimu, uhaba wa wafanyakazi pamoja na gari ya kubebea wagonjwa (Ambulance) Hali inayosababisha kukosekana kwa huduma bora.

Farida Breki Karama, Muuguzi Mzambarauni, amesema Ili kuhakikisha idadi ya mama wajawazito wanajifungulia katika vituko vya afya wamekuwa wakitoa elimu katika jamii hasa maeneo ya Vijiji ambako ndiko kwenye idadi ya Akina mama wanaojifungua majumbani.

Mradi huo wa miaka miwili ambao umeanza mwezi July 2024 na kutarajiwa kukamilika Mwezi December 2026 unaendeshwa na Jumuiya ya kupunguza umasikini na kuboresha Maisha ya watu Pemba (PEPOHUDA) na kufadhiliwa na Shirika la Y+Global kupitia mfuko wa HER VOICE FUND



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...