Skip to main content

"VITISHO VISIWE SABABU YA KUTOKUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI" MKURUGENZI TAMWA, ZNZ

 Na, Thuwaiba Habibu

 


Mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar Dkt Mzuri Issa Ali amewataka wanawake   kutokuogooa vitisho kutoka kwa mtu yoyote ili kuweza kupambania ndoto zao za kuwa viongozi .

Ameyasema hayo huko katika ukumbi wa mkutano Tunguu,Unguja  katika kikao na wadau mbali mbali kujadili  namna gani wanawake wanapata ulinzi dhidi ya ukatili wa kijinsia mitandaoni

Alisema kuwepo kwa vitisho kumewafanya wanawake kuacha kugombe ikiwemo  kukatazwa, kuvunjwa moyo, kukemewa na tuhuma kutoka mitandaoni ambazo bado zina wadhalilisha na kurejesha nyuma juhudi zao katika kugombea.

"Wanaume hutumia uongo kumchafua mwanamke kwasababu jamii inaamini yeye ni mtu ambaye atakiwi kuwa na doa basi ni rahisi kumkosesha."

Kwa upande wake Afisa Sheria Mwandamizi wa Vyama  Vya Siasa Abdul razak Said Ali amesema  kuwepo kwa asilimia 50 baina ya wanawake na wanaume ni harakati za muda mrefu na sasa zinaendelea  ili kuwe na uwiano sawa.

Alisema kupitia  tamko la jumuiya ya Maendeleo la Nchi za kusini mwa Afrika( SADC) la mwaka 2005 na itifaki ya maendeleo ya jinsia 2008  imetekeleza  kiwango cha chini cha ushiriki wa wanawake kwa 30%na baadae  kuimarishwa hadi 50% 

 Aidha alisema changamoto ya uchumi ni  kikwazo kwa wanawake   katika shughuli za kisiasa ni lazima kila chama kitenge bajeti itakayowezesha wanawake  kufikia malengo yao.

"Mfumo wa uteuzi katika vyama vya siasa unaathiriwa kwa kiasi kikubwa na ule wa kifedha ambapo wanawake wengi hukosa fursa," alieleza abdul razak.

Nae Afisa kutoka Malaka ya kupambana na rushwa na Uhujumi uchumi Zanzibar (ZAECA) Yussuf Juma Suleiman amesema  moja ya sababu ambazo zinawakwamisha  wanawake  katika kugombea nafasi za uongozi ni rushwa ya ngono

Amesema kuwa, kabla wanawake hawajaingia katika kugombea nafasi za uongozi, ni vizuri kupewa elimu ya uraia, ili kujua miiko na misingi ya uongozi, ili wasiwe na mwanya wa kutoa rushwa.

Aidha amesema kuwa, serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepitisha sheria mpya ya kuzuia rushwa na uhujumu wa uchumi, sheria namba 5 ya mwaka 2023, kifungu cha 53.

Amesema, kifungu hicho kimeharamisha rushwa ya ngono, kwa kukataza mtu yoyote kushawishi, kuahidi kufanya ngono na adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka saba na kisichozidi miaka 10

“Rushwa ya ngono ni uhalifu kama ulivyo mwingine, na serikali imeazisha sheria ili kukabiliana nayo, lakini wandishi wa habari toeni elimu ili wanawake wanaotia nia wasiwe ni mwanya wa kutokea rushwa,’’ alisema.

 Nae  mdau Mwatima Issa, Rashid alisema kila mtu anatakiwa akipe tamani kitu anachofanya ili kufikia  malengo aliojiwekea kwani ukiwa unajikubali  utafika mbali.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...