Skip to main content

"Tuhamasishe watoto wa kike kushiriki michezo kuleta usawa wa Kijinsia katika sekta zote" Afisa Programu Tamwa, ZNZ


Na, Thuwaiba Habibu, Unguja

Katika kuazimisha siku ya kimataifa ya mtoto wa kike duniani, wadau wa michezo kwa maendeleo Zanzibar ambao ni Jumuiya ya wanasheria wanawake, Zanzibar (ZAFELA) kituo cha mijadala kwa vijana (CYD)na chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA,ZNZ) kwa kushirikiana na shirika la Ujerumani (GIZ) imeandaa shughuli mbali mbali za michezo kwa maendeleo ili kuhamasisha ushiriki wa watoto wa kike na ustawi wa kijinsia katika michezo.

Akitoa taarifa hizo kwa waandishi wa habari Afisa Program wa michezo kwa maendeleo kutoka Tamwa Zanzibar, Khairat Haji amesema maadhimisho hayo yatawashirikisha wanafunzi kutoka skuli mbali mbali za msingi za mkoa wa kaskazini 'A', Mjini ,na Magharibi 'A', na yataanza kwa michezo ya mpira wa pete (Netball) za kirafiki zitakazo husisha timu za watoto wa kike kutoka tumbatu, jongwe,mkokotoni,mto wa pwani, kianga,mtoni , kiembe samaki B' na uroa.

Alisema kuwa shughuli nyengine zitakazo fanyika ni ziara kwenye skuli mbali mbali ili kuendeleza michezo kwa maendeleo (S4 D) ambayo itawafundisha wanafunzi namna ya kujikinga dhidi ya ukatili wa kijinsia pamoja na kuelimisha kuhusu masuala ya wanawake na uongozi.

Amesema kuwa,Wanafunzi pia watashiriki kwenye uchoraji wa picha ambazo zitaakisi maudhui ya S4D ambayo itawapa fursa ya kuelezea mawazo yao, kuhusiana na michezo na usawa wa kijinsia.

Aidha Afisa huyo, amesema kuwa,kilele cha maadhimisho hayo, kitafanyika siku ya jumamosi oktoba 12 mwaka huu,ambapo zitachezwa mechi za fainali ya mpira wa pete,na pia picha zilizochorwa na wanafunzi hao, zitagaiwa kama zawadi.na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni naibu waziri wa maendeleo ya jamii jinsia,wazee na watoto, mheshimiwa Anna Athanas Paul ambae ataongoza shughuli ya kugawa zawadi kwa washiriki wote.

Aidha amesema kuwa, maadhimisho hayo yanalenga kuinua ari ya watoto wa kike kushiriki michezo, kupinga ukatili wa kijinsia na kuboresha usawa wa kijinsia visiwani Zanzibar.

"Tunaamini maadhimisho hayo ni sehemu ya mikakati ya wadau wa SFD Zanzibar,wa kuendeleza uawa wa kijinsia na haki za mtoto wa kike kupitia michezo"" alisema.

Nao, waandishi walioshiriki katika kikao hicho, waliuliza kuwa wamezingatia vigezo gani katika kuzipata hizo shule zitakazo shiriki katika madhimisho hayo.

Akijibu suala hilo, Afisa kutoka CYD Rahma Juma amesema, kuwa katika programu hiyo wanashirikiana na Serikali hivyo, uteuzi wa shule hizo umefanya na Wizara ya Elimu na mafunzo ya Amali Zanzibar.



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...