Skip to main content

MWALIMU WA MADRASA MBARONI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MWANAFUNZI WAKE

 NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba linamshikilishia Ali Shavuai Ramadhan 25, ambaye ni mwalimu wa Madrasa anayeishi Wesha Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake mwenye umri wa miaka 14

Baba wa kambo wa Msichana ambaye jina limehifadhiwa, amesema aligundua kuchelewa kurudi nyumbani kwa binti yake huyo wakati wa usiku na kuchukua hatua za kumuuliza alikuwa wapi na baada ya maswali kadhaa msichina huyo akajibu kuwa alikuwa mwalimu wake wa madrasa nyumbani na kukiri kufanyiwa kitendo cha ubakaji

“Alichelewa kurudi nyumbani akarudi kama muda wa saa 3 hivi nikamuita na kumuuliza ulikuwa wapi? Akanijibu nilikuwa na mwalimu Ali nikamuuliza usiku mulikuwa munafanya nini na mwalimu Ali? Akawa anasita kunijibu, nikaamuliza tena usiku mulikuwa wapi? Akajibu nyumbani kwake, nikamuuliza mulikuwa munafanya nini? Baada ya muda kupita ndipo akanijibu kuwa ni kweli wamefanya hicho kitendo zaidi ya mara moja” amesema baba mdogo wa msichana huyo

 

Akieleza namna walivyotegua mtego uliopangwa na familia ya mtuhumiwa ili kuivirigiza kesi hiyo, Baba mdogo wa msichana huyo amesema “Tulipata taarifa kuwa binti yetu amefanyiwa vitendo vya udhalilishaji na Ali Shavuai Ramadhani ambaye ni mwalimu wake wa madrasa lakini wanapanga mpango wa kumpanga binti yetu amsingizie kijana mwengine ambaye ni mdogo kiumri ili kesi hiyo ionde ke kwa huyo mwalimu na ihamie kwa huyo kijana mdogo ili isiwe na uzito kwa kuonekana wote ni Watoto sisi baada ya kugundua mpango moja kwa moja tukaenda kutoa taarifa Jeshi la Polisi na kushikiliwa wote wawili huyo kijana aliyesingiziwa na huyo mwalimu lakini baadae yule kijana aliachiwa baada ya kuonekana hakuna ishara ya kutenda kosa”

Mwandishi wa Habari hizi alifanikiwa kuzungumza na msichana huyo ili kupata kauli yake dhidi ya tuhuma zakufanyiwa vitendo hivyo vya ubakaji ambapo alikiri kufanyiwa kitenda hicho kwa nyakati mbili tofauti na mwalimu wake

“Ni kweli tumefanya siku mbili alikuwa anatutuma tukamchotee maji kisha tumpelekee nyumbani kwake sasa kuna siku nilikwenda na mwenzangu kisha akamuambia mwenzangu ende zake kisha nikabaki peke yangu tukafanya” amesema

Ndani ya kipindi cha miaka miwili 2022/2024 hii ni kesi ya tano Kisiwani Pemba inayohusisha walimu wa Madrasa kuwafanyia vitendo vya ubakaji wanafunzi wao.




Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...