Skip to main content

"MDIPAO" YATOA ELIMU YA UDHALILISHAJI NA MIGOGORO YA ARDHI, MICHENZANI.

Wananchi wa Shehia ya Michenzani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, wametakiwa kuachana na tabia ya muhali na badala yake kuviripoti vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa Kijinsia ili kupambana na vitendo hivyo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Mkoani (MDIPAO) Hakim Nassor huko Michenzani katika Mkutano kati ya Wasaidizi wa Sheria wa Jumuiya hiyo na Wananchi, amesema miongoni mwa sababu kukoma kwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa Kijinsia katika jamii ni muhali pindi vitendo hivyo vinapotokea.

Akiwasilisha mada ya udhalilishaji na ukatili wa Kijinsia Hakimu Mahakama ya Wilaya Mkoani ambaye pia Hakimu dhamana wa Mahakama ya Wilaya Mkoani Suleiman Said Suleiman amewataka Wananchi walioshiriki katika Mkutano huo kutokuwasafisha watoto pindi wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji Ili kusaidia katika ushahidi makosa hayo.

"Tafadhalini sana musiwasafishe watoto wenu pindi wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji kwani mukiwasafisha munachangia kuondosha ushahidi katika uendeshaji wa makosa hayo" amesema 

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo katika Mahakama ya Wilaya Mkoani Nasim Faki Mfaume, amesema miongoni mwa kesi zinazoripotiwa kwa wingi katika Mahakama mbali mbali ni kukithiri ni migogoro ya Ardhi na kuwataka Wananchi kuwa nyaraka sahihi za umiliki wa Ardhi Ili kuepukana na migogoro ya mara kwa mara.

Hakimu Nasim, aliongeza kuwa sababu zinachangia kuongeza kwa migogoro ya Ardhi ni wamiliki na wauzaji kukosa nyaraka halali za umiliki wa Ardhi hali inayosababisha kuibuka kwa migogoro katika jamii



"Utafiti unaonesha migogoro mingi ya Ardhi inasababishwa na wamiliki na wauzaji wa Ardhi kutokuwa na nyaraka halali za umiliki wa maeneo wanayomiliki au kuuza, na hii inasababishwa na wale wamiliki wa mwa zo Yani mababu zetu kutokuwa na nyaraka halali pamoja na kuacha wasia wa kumiliki Ardhi na kutokurithishwa wahusika pindi wazee hao wanapofariki" amesema 

Bahati Khamis Sharif 45, na mama wa watoto 6 ni miongoni mwa Wananchi walioshiriki Mkutano huo, ameomba kufanyiwa marekebisho kwa Sheria ya mtoto kwani Sheria hiyo ina mapungufu na inachangia kukithiri kwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa Kijinsia katika jamii.

"Kuna kesi ilitokea hapa mtaani mtoto wakike wa miaka 14 amefanyiwa vitendo vya udhalilishaji na Vijana wakiume wenye miaka 17 kesi ikaenda Mahakamani lakini mwisho wa siku wale Vijana walikiri kutenda makosa wapewa adhabu ya kulipa faini na fidia kwa familia ya muhanga lakini mpaka muda huu nazungumza hawajalipa fidia Wala faini jamani hii ni haki kweli, hebu tupeni ufafanuzi wa jambo kama hili" Bahati Khamis Ali, alihoji

Khatib Ussi Hamad, Rawali miaka 84, amesema kuongeza kwa vitendo viovu katika jamii ni kukosekana kwa malezi ya pamoja.

"Zamani malezi yalikuwa ni ya jamii yote Yani mtoto wangu analelewa na watu wote mtaani akifanya kosa Mzee yeyote anaweza kumrudi na akija nyumbani analia akiulizwa unalilia nini hana majibu mazuri anatandikwa tena mbona tulinyooka vizuri lakini sasa hivi kila mzazi na mtoto wake na ndio kama hivi tunashindwa maana hakuna malezi ya peke yako" alisema

Akitoa ufafanuzi kuhusu suala hilo Hakimu Mahakama ya Wilaya Mkoani ambaye pia Hakimu dhamana wa Mahakama ya Wilaya Mkoani Suleiman Said, amekiri mapungufu yaliyomo kwenye Sheria ya mtoto kwani adhabu ya kulipa fidia na faini ambazo zinapaswa kulipwa na wazazi hazisaidii katika kuwarekebisha watoto hao

"Sheria hii imesema endapo mtoto atakutwa na hatia ya kosa la udhalilishaji wazazi wake ndio wanapaswa kulipa fidia na faini Sasa shida inatokea wazazi wengi hawalipi hizo fidia na faini na Sheria haijasema kuwa kama hawakulipa washikwe na kuwekwa ndani" alifafanua

Iddi Thani Suleiman, amesema miongoni mwa changamoto zinazoikabili ni kuhidhiwa kwa maeneo mengi ya Ardhi na wawekazaji Hali inayosababisha Wananchi kukosa maeneo ya kufanyia shughuli zao za kila siku

Miongoni mwa hoja iliyoibuliwa ni Dawati la kusikiliza malalamiko dhidi ya Akina Mama na watoto kwamba inachangia kuporomoka maadili ya watoto katika jamii kama anavyosema, Mohammed Ali Mbwa maarufu kwa jina la Zabadi "Sasa Kuna haya madawati ya Akina Mama na watoto nayo yanachangia kwa kiasi Fulani kuharibu maadili yetu maana ukimgusa mtoto unaenda kushitakiwa na mara unafungwa Sasa hatujui hata tufanye nini" alihoji

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo katika Mahakama ya Wilaya Mkoani Nasim Faki Mfaume, amefafanua "Hiyo hoja ipo sana mitaani lakini niseme kwa kimywa kipana hapa kuwa hakuna Mahakama yoyote hapa Zanzibar imewahi kupokea kesi ya aina hiyo kwamba Kuna mzazi ambaye amefunguliwa kesi kwasababu amemuadabisha mtoto kama kwa mujibu wa Sheria ila ukimuhukumu kiasi ya kumjeruhi au kumvunja hapo ndipo unaweza kufunguliwa mashtaka kwasababu umemuathiri badala ya kumuadabisha" 



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...