Skip to main content

"BADO KUNA UNYANYASAJI MKUBWA WA KIJINSIA KATIKA VYAMA VYA SIASA" DK. MZURI




Na, Hassan Msellem - Pemba 

MKURUGENZI wa Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, amesema bado Kuna vitendo vya unyanyasaji wa Kijinsia katika vyama vya siasa jambo linalosababisha Wanawake kukosa haki yao ya kuwa Viongozi.

Dk. Mzuri ameyasema hayo leo Oktoba 1, 2024 ukumbi wa mikutano wa chama hicho Tunguu Unguja, katika kikao na Wadau mbali mbali kujadili namna gani  wanawake  watapata ulinzi dhidi ya ukatili wa kijinsia  mitandaoni, kupitia mradi wa wakuwawezesha waandishi wa habari vijana.

Amesema kuwa, katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kuna Ripoti kadhaa zinazoonesha unyanyasaji dhidi ya Wanawake waliotia nia nagombea nafasi mbali mbali za Uongozi ndani na nje ya chama Hali inayorudisha nyuma ndoto na juhudi za wadau katika kufikia azma ya 50 kwa 50 kwenye vyombo vya kutunga Sheria.

"Licha ya kazi kubwa inayofanywa na wadau katika kuhakikisha usawa wa Kijinsia unafikiwa katika vyombo vya maamuzi bado Kuna malalamiko makubwa kutoka kwa Wanawake wakilalamikia manyanyaso na vitosho kutoka katika vyama vyao hususan kipindi cha Uchaguzi" amesema 

Dr. Mzuri pia amesema suala la unyanyasaji wa Kijinsia mitandaoni ni miongoni mwa changamoto zinazoikabili Wanawake katika kutimiza ndoto zao zakushika nafasi mbali mbali za Uongozi na kusema "Kuna hili suala la unyanyasaji wakimtandao nalo ni miongoni mwa changamoto zinazowakabili Wanawake wengi kutokufikia malengo kwani suala hili limekuwa likijitokeza mara kwa mara na chakusikitisha zaidi Mamlaka ambazo zinajukumu la kukabiliana na suala hili zinaonekana kutokulipa kipaumbele katika kukabiliana nalo" 

Aidha Dr. Mzuri amewataka Wanawake licha ya kukumbana na manyanyaso na vitosho kutokuogopa na badala ya kujiona upya kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 Ili kuongeza idadi ya Viongozi Wanawake katika vyombo vya kutunga Sheria.


Afisa kutoka Mamlaka ya kuzuia rushwa na uhuhumu wa uchumi Zanzibar ‘ZAECA’ Yussuf Juma Suleiman, amesema moja kati ya vikwanzo  vinavyowarudisha nyuma  wanawake katika kugombea nafasi za uongozi ni rushwa ya ngono.

Amesema kuwa, kabla wanawake hawajaingia katika kugombea nafasi za uongozi, ni vizuri kupewa elimu ya uraia, ili kujua miiko na misingi ya uongozi, ili wasiwe na mwanya wa kutoa rushwa.

Aidha amesema kuwa, serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepitisha sheria mpya ya kuzuia rushwa na uhujumu wa uchumi, sheria namba 5 ya mwaka 2023, kifungu cha 53.

Amesema, kifungu hicho kimeharamisha rushwa ya ngono, kwa kukataza mtu yoyote kushawishi, kuahidi kufanya ngono na adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka saba na kisichozidi miaka 10.

“Rushwa ya ngono ni uhalifu kama ulivyo mwingine, na serikali imeazisha sheria ili kukabiliana nayo, lakini wandishi wa habari toeni elimu ili wanawake wanaotia nia wasiwe ni mwanya wa kutokea rushwa,’’ alisema.

Nae Afisa sheria Mwandamizi kutoka ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, Abdul-razak Said Ali amesema   serikali imekuwa ikichukua jitihada mbali mbali, katika kumuwezesha mwanamke kugombania nafasi za uongozi ili kuongeza ushiriki wao.

Alisema kuwa, moja ya hatua iliyochukuliwa na serikali ni kuongeza kifungu katika sheria ya vyama vya siasa nambari 1 ya mwaka 2024, kifungu namba 10 (c) ndani ya marekebisho, kinatoa masharti yanayohusiana na uanzishwaji wa dawati la kijinsia na ushirikishwaji wa jinsia na jamii.

Na washiriki wa mkutano huo Mwalim Mwatima Issa, Rashid alisema wandishi wa habari wanatakiwa kujipa kipaumbele katika kufanya kazi zao.

Nae mshiriki Nusra Shabani aliuliza kwanini vyama vidogo vya siasa, havipewi ruzuku ili kuviwezesha vishiriki kikamilifu katika uchaguzi.

                Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...