Skip to main content

“SMILE PEMBA MARATHON” KUBORESHA USTAWI WA WATU WENYE ULEMAVU

 Na, Hassan Msellem- Pemba


Wananchi Kisiwani Pemba wametakiwa kushiriki mashindano ya Mbio yanayobeba jina la Smile Pemba Marathon ili kufanikisha lengo la Mbio hiyo.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Ahmed Abuubakar Mohammed huko Gombani Pemba, amesema lengp la Mbio hizo ni kukusanya fedha kwa ajili ya kununua vifaa tiba na vifaa saidizi kwa watu Wenye Ulemavu.

Aidha amesema Mbio hizo za hisani zinatarajiwa kufanyika mwezi Novemba 2024, katika Uwanja wa Gombani Pemba kwa kukusanya wanariadha kutoka ndani na nje ya Nchi, ambapo Mgeni rasmi wa mbio hizo anatarajiwa kuwa makamo wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdalla

“Naomba nitowe wito wangu kwa wananchi Watanzania wote wapenda maendeleo kuweza kushiriki katika mbio hizi na pia kuweza kutoa michango yao kwa ajili ya kusaidia Watu Wenye Ulemavu” amesema

Aliongeza kuwa Mbio hizo zinatarajiwa kuwa mbio za Nusu Marothon zikijumuisha mbio za Kilometa 21, Kilometa 10 na Kilometa 5 sambamba na mbio za Baiskeli ya magurudumu matatu (Tricycle Racing) ambazo zinatarajiwa kuanza saa 12:30 Asubuhi

Kwa upande wake Meneja Mkaazi Pemba wa Kampuni ya TTCL Khamis Is-haka Ngwali, amesema wamemua kuwa wadau wa Mbio hizo kwa lengo na kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha hali za watu wenye ulemavu zinaimarika

Amesema “Licha ya kufanya biashara tumeguswa na programu hii ya wenzetu wa SMILE ya kuwasaidia ndugu zetu wenye mahitaji maalum programu hii ya kuchangisha vifaa itawasaidia ndugu zetu hawa wenye uhitaji maalum kupata vifaa au nyezo kwa mfano ukimsaidia kigari mtu mwenye Ulemavu umemsadia nyezo ya kusafiri na kufanya shughuli zake za kimaendeleo na kujenga Uchumi wetu kwahivyo kama taasisi ya Umma tumeshiriki katika hili zoezi kuwajengea uwezo wenzetu hawa wenye ulemavu wapate vifaa ili waweze kufanya shughuli zao za kimaisha ikiwa ni sehemu ya kuiunga mkono Serekali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar”

Arif Mohammed Said, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Pemba, amesema kwa dhati wamekubali kuunga juhudi za Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamo wa kwanza wa Rais kwa kuchangia vifaa tiba na vifaa wezeshi kwa watu wenye Ulemavu Ili kuweza kuwawezesha Watu Wenye Ulemavu ambao ni sehemu ya walipa Kodi.

Sambamba na hayo Meneja huyo amewataka Wananchi kuachana na dhana kwamba Kodi zinazokusanywa Zanzibar haziwanufaishi Wazanzibari na badala yake kufahamu kuwa taasisi zote za Kodi za TRA na ZRA zinafanya kazi ya makusanyo kwa mujibu wa Sheria na kwamba Kodi hizo zinatumika kwa maslahi ya Wananchi wote wa Bara na Visiwani.

Gharama za usajili wa Mbio hizo ni shilingi elfu thelathini za Kitanzania kwa kila mshiriki na kwa upande wa wawashiriki wan je Tanzania ni Dola 10, ambapo gharama za malipo zitafanyika kwa njia ya simu kupitia kwenye nambari 15115602 Tigipesa yenye jina la Smile Pemba Marathon

Mbio za Kilometa 21 zitaanzia Gombani Kongwe, kupitia Mjini Chake Chake, Afrikana, Kichungwani, Qatar, Tibirinzi, Pondeani, Pagali na Kumalizia Gombani Mpya, Mbio za Kilometa 10 zitaanzia Gombani Kongwe kutipia Machomane, Msingini, Tume huru ya Uchaguzi, Sukita, Banki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Machomane na kumalizia Gombani Mpya.

Kilometa 5 Mbio zitaanzia Gombani Kongwe, kupitia Machomane, Msingini, Tume huru ya Uchaguzi, Sukita, Banki, Machomane na kumalizia Gombani Mpya, na kwa upande wa Mita 100 ambazo ni kwa ajili ya Watu wenye Ulemavu zitafanyika ndani ya Uwanja wa Gombani.

Wadau wa Kuu wa Mbio hizo ni Kampuni ya simu ya TTCL, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA)

Zawadi za washindi wa Mbio hizo zitatangazwa mara tu utaratibu wa ugawaji wa zawadi hizo utakapo kamilika.

Kwa mawasiliano zaidi kuhusu Mbio hizo unaweza kupiga simu nambari

+255773538539 au +255777671211 au +255773818117



Mwisho

 

 

 

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...