Skip to main content

Unyanyapaa unavyokatisha ndoto za watoto wa kike wenye ulemavu kwenye michezo.

NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA



Katika jamii nyingi kumekuwa na tamaduni ambazo zimekuwa zikiwanyima fursa watu wenye ulemavu wakiwemo wanawake katika kushiriki kwenye michezo kwa kile wanachodhani kuwa watu hao kuwa hawana uwezo wa kushiriki michezo.

Pamoja na juhudi zinazochukuliwa Serikali na wadau mbali mbali katika kuondosha changamoto hiyo lakini bado wapo baadhi ya wanajamii na  uwazi wa uthubutu katika kuwapambania watu hao kwenye mambo ya msingi ikiwemo elimu na hata kushiriki katika michezo.

Rashid Hamad Khamis, ni Katibu wa timu ya watu wenye Ulemavu Mkoa wa Kaskazini Pemba, alisema jamii haijatilia mkazo kwa watu wenye ulemavu wa akili katika kushiriki michezo hali inayosababisha kundi hilo kuachwa solemba kwenye michezo.

"Miongoni mwa madai ya wazazi juu ya kutowaruhusu kuingia kwenye michezo ni pamoja na kutokuwaamini juu ya mazingira yao  kutokana na ulemavu wao jambo  linawanyima haki hiyo ya kushiriki kwenye michezo" alisema katibu huyo

Akizungumza juu ya namna ya  walivyo jiandaa  alisema kuwa  hivi sasa wameandaa utaratibu maalumu wa kuwapitia wazazi kuwaelimisha wazazi wa watoto wenye ulemavu ili kuwapa uelewa juu ya watoto hao kushiriki kwenye michezo

"Tunajaribu kuwafahamisha Wazazi wa watoto wenye ulemavu  kuwa  kuwanyima fursa ya kushiriki michezo  watoto hao ndani ya jamii  bado  ni tatizo kubwa ambapo  bila ya  kutambua kuwa ni  kuwanyima haki zao  pamoja na kuwanyanyapaa" alisema.

Hata hivyo alisema ingawa  kwa sasa  wameweza kuanzisha timu moja tu ya watu wenye ulemavu kwa wanaume lakini kutokana na umuhimu huo wataanzisha   timu maalumu ya Wanawake

"Katika msimu  ujao tumeandaa mashindano ya watu wenye ulemavu kwa  timu mbili za wanawake na wanaume  ili kwa lengo la kutoa haki sawa ya michezo kwani kufanya hivyo kutayaweka karibu na jamii makundi hayo  ambayo yamesahaulika"  aliongeza

Mratibu wa Baraza la Watu Wenye Ulemavu Kisiwani Pemba Mashavu Juma Mabrouk, ameeleza kuwa wamekuwa wakielimisha jamii juu ya namna ya kuishi na watu hao kwa  kuwashirikisha katika mambo mbali mbali ikiwemo kushiriki katika  michezo.

Alisema baraza lina  jukumu la  kuwasajili na kuwatambua pamoja na kuwasaidia kwa vitu mbali kupitia watu ambao wamekuwa wakiwatafuta kuyaangalia makundi hayo.

"Sisi Baraza la Watu wenye ulemavu tumekuwa na jumuku la kuwasajili kuwatambumbua ili lengo letu nikuona watu hao wanasaidiwa,tumekuwa tukitafuta watoto wa  aina hiyo" alisema.

Alinena mara nyingi makundi ya watu hao yamekuwa yakiwekwa nyuma na kukoseshwa haki zao za msingi lakini baraza limekuwa likiwakutanisha na watu tofauti kutoa elimu ya kutokulibagua kundi hilo

Amesema kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar,ya Mwaka 1984 kifungu 12 (1) kina fafanua kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria na wanayo haki bila ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa.

Shekh Naasor Abdalla Mauli  ni Mwanaharakati  wa mambo mbali mbali ya kijamii yakiwemo ya usawa wa kijinsia amesema Dini ya Kiislamu imehimiza suala la usawa kwani wanadamu wote ni sawa licha ya tofauti zao za kimaumbile

Mratibu wa Chama Cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania Zanzibar,Ofisi ya Pemba Fthiya Mussa Said, aliongeza kuwa Tamwa imekuwa ikitunana na wadau mbali mbali katika kushajihisha wanawake kupewa fursa na kama wanaume katika kushiriki michezo.

Alisema ukiangalia duniani wanawake wengi wamekuwa wakionekana kwenye mashindano tofauti hali hiyo inaonesha wanawake wanaweza lakini kwa upande wa Pemba,bado jamii inawanyima nafasi wanawake kushiriki michezo.

Waziri Tabia anasema, kwa upande wa michezo ya watu wenye ulemavu wa mguu mmoja na mkono mmoja, Wizara imefanikiwa kulisaidia Shirikisho la mchezo huo, kushiriki mashindano ya Kitaifa yaliyofanyika Arusha.

Lakini hata Shirikisho la michezo ya Viziwi Zanzibar (SHIMIVIZA) limesaidiwa kuandaa bonanza, kwa ajili ya shamra shamra ya kuadhimisha siku ya viziwi duniani.

Sheria ya watu wenye ulemavu namba 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (9) kimesema watu wenye ulemavu wanayo haki ya kushiriki kwenye michezo na burudani.

TAMKO LA SERA YA MICHEZO YA MWAKA 2018

Serikali itahakikisha Watu Wenye Ulemavu wanawekewa mazingira yanayofaa, kuwawezesha kupata fursa sawa na haki ya kushiriki mashindano mbali mbali kwa uwezo wa hali zao.

 

MWISHO.

 

 

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...