Skip to main content

"UCHUMI WA BULUU NI BIASHARA KATI YA SERIKALI NA BENKI YA CRDB CRDB" MWENYEKITI WA ADC TAIFA-SHABANI ITUTU.

Na, Hassan Msellem, Pemba 


Mwenyekiti wa chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) Taifa Shabani Itutu, ameiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Uchumi wa Buluu kuboresha hali za Wananchi kupitia Sera ya Uchumi wa Buluu, ambayo mpaka sasa haijafikiwa ipaswavyo.


Mwenyekiti huyo ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wanachama wa wa Chama cha ADC na Wananchi mbali mbali Kisiwani Pemba, amesema licha ya Serikali ya awamu ya nane kuanzisha Sera ya Uchumi wa Buluu kwa lengo la Kuboresha Hali za Wananchi kupitia rasilimali za baharini ikiwemo uvuvi wa Samaki na zao la mwani bado hali za Wananchi kupitia rasilimali hizo hazijaimarika.



Akitaja sababu zinazobabisha kutokufikiwa kwa Sera ya Uchumi wa buluu kwa Wananchi ni pamoja kukosekana kwa vyombo vya kisasa vya uvuvi, kukosekana kwa viwanda vya kusindika samaki pamoja kutokufanya kazi kwa viwanda vya kuchakata zao la mwani.



"Tunaamini dhamira ya Serikali ni njema sana kupitia Sera ya Uchumi wa Buluu lakini dhamira hiyo haiwezi kufikiwa endapo Serikali itashindwa kununua meli za kisasa zinazoweza kwenda kwenye kina kirefu cha maji, kuwa na uwezo mzuri wa kuhifadhia tani za kutosha za kuhifadhia samaki pamoja kuwa na viwanda vya kusindika samaki, pamoja kufanya kazi kwa viwanda vya kuchakata mwani ambavyo vimezinduliwa hivi karibuni" alisema 



Akifanya ziara katika kaburi la aliyekuwa Makamo wa kwanza wa Rais Zanzibar Marehemu Mwalim Seif Sharif huko Mtambwe Nyali, amewataka wanasiasa na watendaji wa Serikali kufuata nyayo za Kiongozi huyo Ili kuwaletea Wananchi Maendeleo bila ya ubaguzi.



"Naomba niwasihi sana viongozi vyama mbali mbali vya siasa pamoja watendaji wa Serikali kuenzi na kufata nyayo za marehemu Maalim Seif Sharif Hamad katika kuwatumikia Wananchi, Marehemu hakuwa na misingi ya ubaguzi Wala dhulma katika kipindi Chake chote cha kuwatumikia Wananchi na ndio maana leo tunamuenzi kwa heshima kubwa"


Kwa upande wake Katibu wa chama cha ADC Taifa Mwalimu Hamad Azizi, amesema chama cha ADC ni miongoni mwa vyama 19 Tanzania vilivyopatiwa Usajili kikiwa na miaka 13 tangu kuanzishwa kwake, hivyo basi amewataka Vijana na Wananchi kujiunga na Chama hicho Ili kunufaika na Sera, Ilani, malengo yanayotokana na Chama hicho.


Akitoa ufafanuzi kuhusu ubovu wa barabara ya Mtambwe Nyali Hadi Uondwe, amesema tayari Uongozi wa Chama hicho umeshazungumza na Serikali Ili kuhakikisha tatizo la ubovu wa barabara hiyo linatatuliwa.


Nao baadhi ya Wananchi waliohudhuria katika ufunguzi wa TAWI la Chama hicho huko Mtambwe, wamesema wanakabiliwa na tatizo la ubovu wa barabara hali inayowasababisha kushindwa kufanya shughuli zao zakimaisha ipaswavyo.


"Kwakweli changamoto yetu kubwa ni ubovu wa barabara tunapata shida sana sio kwa kipindi hichi cha jua wala mvua kwasababu Barabara ni mbovu sana hata hivyo vinavyokuja huku vinaharibika Kwahivyo inatubidi tutembee kwa miguu kwenda kwenye shughuli zetu mbali mbali" alisema mmoja wa Wananchi hao


Katika Ziara hiyo ya ufunguzi wa matawi mwenyekiti wa ADC Taifa Ndugu Shabani Itutu alifungua TAWI la Chama cha ADC Kinazini, na Nyali huko Mtambwe, Tawi la ADC Jombwe na Chole Kengeja, na kuwakabidhi kadi za uanachama kwa viongozi na wanachama wa matawi hayo pamoja na kutembelea kaburi la aliyekuwa Waziri Kiongozi Dr. Omar Ali Juma Mgogoni na aliyekuwa Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad huko Mtambwe Nyali.



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...