Skip to main content

WANAWAKE PEMBA WATAKIWA KUSHIRIKI MCHEZO WA KUOGELEA ILI KUNUFAIKA NA FURSA ZINAZOTOKANA NA MCHEZO HUO.

Wanawake Kisiwani Pemba wametakiwa kushiriki katika mchezo wa kuogelea ili kunufaika na fursa za kiuchumi zinazotokana na mchezo huo.


Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Khatibu Juma Mjaja wakati akikabidhi zawadi kwa washindi na washiriki wa Bonanza la kuogelea huko katika viwanja vya burudani Furaha Mini Foro Pemba, amesema kupitia mchezo wa kuogelea kuna fursa nyingi za kiuchumi hivyo wanawake wanatakiwa kushiriki katika mchezo huo ili kunufaika na mchezo huo.

 

“Mchezo wa kuogelea ni miongoni mwa michezo maarufu sana duniani na una mashindano mengi ya ndani na kimataifa na chakusikitisha wanaoshiriki mchezo huu mara nyingi wanawakuwa ni wanaume hususan katika nchi za Afrika, hivyo basi niwasihi sana akina mama mushiriki mchezo huu kwani una faida nyingi sana ikiwemo faida za kiafya, kujihami, kifedha n ahata kutembea nchi mbali mbali duniani” alisema

 

Sambamba na hayo DC Mjaja amewapa pongezi wanawake watatu kutoka Tumbe Mkoa wa Kaskazini Pemba walioshiriki Bonanza hilo kuwa wanawake wa mfano kwa wanawake wengine Kisiwani Pemba na kuwataka wanawake wengine kuiga mfano wa wanawake hao.

 


“Tukiangalia kwenye Bonanza letu leo tunao wanawake watatu lakini hawatokei hapa Furaha hii inamaanisha kuwa wanawake wa Fuhara na viunga vyake bado hatujahamasika na mchezo wa kuogelea tutafurahi tukiona bonanza la mwakani wanawake wa Furaha, Mvumoni na Vitongoji nao wanashiriki katika bonanza hili” Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja

 


Mkurugenzi wa kampuni ya JAZEERA-MISALI TOURS & SAFARI Salum Khamis Juma, amesema wameamua kutoa fursa kwa wanawake kushiriki katika bonanza hilo ili kuweka usawa wa kijinsia pamoja na kuwahamasisha wanawake wengine kushiriki katika mchezo huo.

 


Kaije Said Bakar ni mkufunzi wa somo la kuogelea kwa wanawake amewataka wanawake wenzake kushiriki katika mchezo wa kuogelea ili kufaidika na fursa za mchezo huo ikiwemo kuwa na afya njema na kujipatia fedha.

 

“Mimi ni mwanamke kama wanawake wengine nina mume na watoto 11 lakini nina uwezo mzuri wa kuogelea nina panda mwani katika kina kirefu cha maji napia nawafundisha wanawake wenzangu kuogelea na kama munavyoona hapa leo kuna wenzangu watatu wameshiriki bonanza hili na tayari wemeshazawadiwa fedha taslim elfu 30 sio kidogo kama wangekuwa wako nyumbani wasingeweza kuipata hiyo, kwahivyo nawasihi sana wanawake wenzangu kushiriki ipaswavyo katika mchezo huu” alisema


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...