Skip to main content

Wanawake waongoza, Tunzo waandishi YMF.

 Habari Na, Ahmed Abdulla.

Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania, TAMWA Zanzibar kimewatunuku vyeti waandishi chipukizi ishirini na nne (24) waliohitimu mafunzo ya kuandika habari za wanawake na Uongozi.


Hafla hiyo ya kuwatunuku vyeti iliofanyika ukumbi wa Bima ulioko Mperani mjni Unguja iliohudhuriwa na wahariri, wadau wa habari pamoja waandishi wa habari kutoka Zanzibar.


Mapema Kaimu Afisa Mradi wa kuwajengea uwezo waandishi chipukizi (YMF) kutoka TAMWA ZNZ Khayrat Haji amesema jumla ya vipindi na Makala 347 kati ya 348 zilikusanywa ikiwemo radio 117, magazeti 47 na mitandao ya kijamii183 zilizojikita katika ushiriki wa nafasi za Uongozi kwa wanawake.


Tumekuwa na program hii kwa kuimarisha nafasi za Uongozi kwa wanawake kwa kutumia vyombo vya habari ambapo waandishi chipukizi (24) wamepatiwa mafunzo yenye kuakisi mabadiliko chanya katika jamii, Khayrat Haji, Kaimu Afisa Mradi.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania, TAMWA ZNZ Dk Mzuri Issa amesema waandishi chipukizi wamesaidia jamii kujua haki zao za msingi hasa wanawake na kuongeza idadi ya washiriki katika ngazi za maamuzi.


“Wanawake wengi wamekuwa na muamko baada ya kutambuwa haki zao, matarajio yetu katika uchaguzi mkuu 2025 wanawake watajitokeza wengi katika majimbo kugombea nafasi za Uongozi, Dk Mzuri Issa, Mkurugenzi TAMWA ZNZ.


Mjumbe wa Bodi TAMWA ZNZ Hawra Shamte amewasihi waandishi wa habari chipukizi kufanya kazi kwa malengo na kufata miiko na maadili ya Tasnia ya habari kwa kufanya kazi na jamii kwa lengo la kuleta mabadiliko nchini.


“Waandishi ni daraja kati ya Viongozi na jamii, pia ni mdomo wa kuwasemea wasiokuwa na sauti hivyo kutumia nafasi hiyo kwa kujitoa na kusaidia jamii, Hawra Shamte, Mjumbe wa Bodi TAMWA ZNZ.


Shifaa Said Hassan Jaji Kiongozi kati ya watatu katika Tunzo waandishi wahabari chipukizi kupitia mradi wa kuimarisha nafasi za Uongozi kwa wanawake kupitia vyombo vya habari amesema katika kazi hiyo wameangalia vigezo muhimu kama vile Uweledi na umahiri wa Uandishi, matumizi sahihi ya lugha, pamoja na upekee wa mada.


“Makundi ya watu wenye mahitaji maalum bado hatujayatendea haki tumeyasahau ni vyema tukajikita kuyafanyia kazi ipasavyo katika habari tunazoandika, Shifaa Said, Jaji Kiongozi.


Meneger kutoka Radio Jamii Mkoani Said Omar amesema mafunzo yanayotolewa na Chama cha Waandishi Wahabari Wanawake Tanzania TAMWA ZNZ kwa waandishi wahabari ni moja kati ya chachu ya mafanikio ya kituo hicho.


“Takribani kwa miaka nane(8) tokea kuanzishwa kwa Radio Jamii Mkoani Pemba, hatujawahi kupokea tunzo, Ila vijana wa YMF wametuheshimisha kutoka TAMWA ZNZ, Meneger Radio Jamii Mkoani Pemba.


Berema Suleiman Nassor ni Mwandishi Chipukizi (YMF) kutoka kituo cha Zenj FM Radio amesema katika kukamilisha majukumu yao kikwazo kikubwa ni upatikanaji wa takwimu hivyo husababisha kuchelewa kumaliza kazi kwa wakati uliopangwa.


Katika Tunzo hiyo mshindi aliefanya vizuri katika kipengele cha Radio ni Amina Masoud kutoka Radio Jamii Mkoani, Hassan Msellem, Mitandao ya Kijamii na kwa upande wa Gazeti ni Asya Mwalim, Zanzibar Leo.


Mradi wa kuwawezesha waandishi wahabari chipukizi (YMF) kuandika habari za wanawake na Uongozi ni wa miaka miwili ,ulioanza mwaka 2022 -2024, uliowashirikisha waandishi ishirini na nne (24) kutoka Unguja na Pemba uliotekelezwa na TAMWA kwa kushirikiana na National Endosment for Democracy (NAD).


MWISHO.


    

   

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...