Skip to main content

Waandishi wa habari chipukizi wapongezwa kwa kutendea haki mradi wa SWIL.

Na, Thuwaiba Habibu.

Mwenyekiti wa kamati ya utetezi kutoka Tamwa Bi shifaa said hassani amewapongeza waandishi wa habari chipukizi kutendea haki mradi wa wanawake na uongozi kwa kufanya kazi kwa kitaalamu zaidi.


Ameyasema hayo katika sherehe ya mahafali ya waandishi wa habari chipukizi yaliofanyika ukumbi wa bima mpira mkabala na kituo cha polisi madema alisema hawa waandishi wa habari chipukizi wameweza kutendea haki mradi wa wanawake na uongozi na kuweza kuibua vitu ambavyo walivisahau kama vipo katika jamii yao na kuweza kuviandikia makala za magazeti vipindi vya Redio na TV.


Alisema tumezoweya kuona makala zinazomuhusu mtu anahojiwa mtu mmoja peke yake lakini wao walitumia vyanzo tofauti tofauti vya habari na kazi zao ambazo amefanywa ziliandikwa kitaalamu kwani wengine kusubutu kutumia mikataba ya kikanda na kimataifa.


Pia aliwataka waandishi hao wasifanye mahojiano marefu ili kuleta ladha zaidi katika makala zao.


Alisema changamoto ambayo niliona ndani ya makala mulizofanya ni mohojiano marefu suala ambalo nimenifanya nijilazimishe kusikiliza na kusoma.


Aidha alisema kwa mwaka huu kidogo waandishi wamelisahau kundi la watu wenye ulemavu na kuwataka waandishi wajisongeze karibu na watu hawa kwani hizi ni sauti za wasio sauti.


"Hata kama hatukuwaweka katika makala zetu basi japo tuwafanyie mahojiano na wao wawe miongoni mwa walioshiriki alieleza"


Nae mjumbe wa bodi ya Tamwa bi Hawra shamte aliwaomba waandishi hao waweze kuwa ngangari na kutekeleza vigezo vyote vya uandishi wa habari kwa kutumia kalamu zao Vizio ili kuhakikisha sauti za wanawake, vijana,watoto na watu wenye ulemavu zinasikika.


Alisema munatakiwa kuwa waadilifu na kufuata maelekezo ya uandishi wa habari na tusifanye kazi kwa kutegemea kitu na tufanye kazi kwa ajili ya kutetea jamii yetu.


Hata hivyo aliwashukuru wahariri na wasimamizi kuwasimamia kufanya utendaji kazi ulio imara.


"Mumeonesha kujitoa na kutuheshimisha kwa kuhakikisha wanawake wanapata nafasi wanazo stahiki na naamini kuwa nyinyi ndio wahariri wa baadae"



Nao wahitimu wa mradi huo Berema Suleman Nassor na Nihifadhi Abdallah Issa walitowa shukurani kwa chama cha waandishi wa habari wanawake Tamwa kwa kuweza kuwapatia mafunzo yaliyoweza kuwafunza namna ya kuandika habari za wanawake na uongozi.


Awali walikuwa hawajuwa kitu gani wafanye katika kukamilisha kazi hii lakini kutokana na mafunzo waliopatiwa waliweza kujuwa kuandika hata kwa kutumia mikataba mbali mbali.


Vile vile walisema kuna changamoto mbali mbali walizokabiliana na lakini walihakikisha wanazishinda ili kukamiliza kazi hizo.


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...