Skip to main content

Timu ya wanawake ya Velleyball na Basketball Pemba, yajipanga na mashindano ya Umitashumta.

 Na, Salim Hamad, Pemba


Timu ya Wanawake ya Mchezo wa Volleyball na Basketball Kisiwani Pemba,ipo katika mchakato wa kujiandaa ya Michuano ya Umoja wa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) inayotarajia kuanza hivi karibuni Mkoani Tabora.

Akizungumza na Mwandishi wa Habari hizi Mratibu idara ya Michezo Pemba,Mzee Ali Abdalla alisema Mashindano hayo yanashrikisha timu mbali mbali kutoka mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani.

Alisema Michuano hiyo hufanyika kila mwaka na kushirikisha michezo tofauti ikiwemo Volleyball, Basketball kwa wanawake na Fotball na Riadha kwa Upande wa Wanaume.

Alisema timu za wasichana zimekuwa zikifanya Vizuri kwenye Mashindano hayo licha ya kuwepo kwa ushindani wa hali ya juu kutokana na timu za Tanzania bara na wao kuwania ushindi wa mashindano hayo lakini  nazo zimekuwa zikipambana.

Alisema ingawa wachezaji wanapofika kule wanapata changamoto ya hali ya hewa kutokana badiri kwenye mikoa hiyo lakini wamekuwa wakipambana na kupata matokeo mazuri.

Alisema katika kipindi cha Mwaka jana timu hiyo ya wanawake kwa upande wa Volball ilishika nafasi ya pili baada ya kuzichapa timu mbali mbali za mikoa ya Tanzania Bara.

‘’Mashinadno haya ya UMITASHUMTA kwa upande wa Shule za Msingi Tanzania na UMMISETA kwa upande wa Shule za Sekondari Tanzania yamekuwa yakifanyika kila mwaka ambapo timu hii ya wasichana ya mchezo wa basket Ball na Voll Ball imeanza maandalizi ya kujiandaa na michuano hiyo’’alisema Mzee.

Hata hivyo Mzee alisema Mashindano hayo yapo Chini ya Wizara ya Elimu yakiwa na lengo kufufua vipaji na kuviendeleza vipaji Vilivopo Mashuleni Tanzania.

Kwa upande wake Mmoja wa Washiriki wa Mashindano hayo Fatma Said wanajipanga kuhakikisha warejesha ushindi Kisiwani Pemba,ili kuijengea sifa Zanzibar, kwa kufanya Vizuri kwenye mashindano hayo makubwa.

MWISHO.

 


Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...