Skip to main content

Msichana mwenye ulemavu wa viungo apewa ujauzito.

 Na, Salim Hamad

Pemba. Mama Mzazi wa Msichana mwenye ulemavu wa Viungo na akili  jin limehifadhiwa mkaazi wa kiuyu Mbuyuni Wilaya ya Micheweni Mkoa Kaskazini Pemba, ameomba Serikali na wadau wa kupinga vitendo vya udhalilishaji kumsaidia ili haki iweze kutendeka kutokana na kitendo cha mtoto wake kupewa.


Akizungumza kwa masikito Mama huyo alisema mtoto wake huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 20 alikuwa hana  tabia ya kutoka nje lakini akamuona mtoto wake huyo anapatwa na uchungu na kujifua.


Alisema walikuwa hawajabaini chochote mshichana huyo kuwa anaujauzito walifikiri kuwa tumbo alilokuwa nilakawaida hata walipokujashtuka tayari kashakuwa karibu na kujifungua.

Alisema hali hiyo ilimpa huzuni kubwa kwa kudhalilishwa mtu huyo mwenye ulemavu aliyekuwa haweze kumfahamu aliyemfanyia kitendo hicho.

‘’Kitendo hichi kimenisikisha sana cha mwanangu Mlemavu kupwa ujauzito na kimenishangaza kitendo hichi kwani mtoto wangu huyo hana tabia ya kutoka nje’’alieleza Mama huyo.

Sheha wa Shehia ya Shanake Kiuyu Ali Hamad Sharifu alisema baada ya kupata taarifa ya hiyo aliifkisha kwa Serikali ya Wilaya hiyo ili kuona hatua stahiki zinachukuliwa kwa alidaiwa kufanya kitendo hicho.

‘’Mimi nilipokea taarifa kutoka kwa wazazi wa Msichana huyo mwenye ulemavu amepewa ujauzito na tayari Alishajifungua ingawa matokea haya tumekuwa tukiyakemea lakini bado yanaendelea kujitokeza’’alisema.

Mkuu wa Wilaya  ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya alilaani kitendo hicho na kueleza kuwa Serikli itaendelea kuchunguza alifanya tukio hiyo ili aweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya aliwata Wazazi hao kuwa makini na kuacha kuwaamini wengine kukaanaye kwani kuna baadhi wamekosa ubinadamu na kutenda Vitendo hivyo.

‘’Nalaani kitendo hichi mtu kama huyo Mlemavu anafanyiwa udhalilishaji anapewa ujauzito ukweli jambo hilo linaumiza sana tutaendelea kufutilia kufahamu alifanya kitendo hichi ili tuweze kuchukua hatua kali dhidi yake’’alisema DC Mgeni’’alisema.

Hata hivyo aliwataka wazazi hao kutoa mashirikiano ya dhati pindi atakapobainika na kupelekwa kwenye Vyombo vya Sheria wasije kubali kufanya suluhu na kuahidi kuisimamia kesi hiyo hadi mtuhumiwa aweze kutiwa hatiani.

MWISHO.

 

Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...