Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2025

Ongezeko la Madiwani Wanawake Vijana 2025, Tumaini Jipya Wanawake kuwa Viongozi.

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA. Ongezeko la madiwani wanawake katika ngazi mbali mbali Mkoa wa Kusini Pemba limekuwa ishara ya mabadiliko ya kijamii, kiuchumi na kisiasa, pamoja na mwamko mpya wa jamii kutambua uwezo wa wanawake kama viongozi bora na chachu ya maendeleo. Miongoni mwa Madiwani Wanawake vijana waliopata fursa ya kuteuliwa kushika nafasi hizo na kuwawakilisha Wanawake wenzako vijana ni pamoja Amria Seif Saleh, ambaye ameteuliwa kuwa Diwani wa Baraza la Mji Mkoani na Fatma Khamis Ali, ambaye ni Diwani wa Wadi Kibokoni Vitongoji, wote wakiwa ni vijana chipukizi katika ulingo wa siasa na uongozi Kisiwani Pemba. Mabadiliko ya Kijamii na Kuongezeka kwa Uelewa k atika kipindi cha miaka ya karibuni, kumekuwa na kampeni mbalimbali zinazoendeshwa na mashirika ya kiraia, Serikali na taasisi binafsi zinazolenga kuongeza ushiriki wa wanawake katika uongozi, Elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa usawa wa kijinsia na nafasi ya mwanamke katika maamuzi imechangia kwa kiasi kikubwa kupungu...
AJISALIMISHA KITUO CHA POLISI KUDAI MTOTO WAKE ALIYEMTUPA. Novemba 15.2025 kipindi Cha Mawio kiliripoti tukio la mtoto mchanga wakike mweye umri wa wiki moja kutupwa huko Kitope ambapo aliyemtupa mtoto hakufahamika Hatimae Jana Novemba 21.2025 Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Tattu Mohamed mwenye umri wa miaka 26, mkaazi wa Mfenesini Unguja, Zanzibar amejisalimisha katika Kituo cha Polisi Mahonda kudai mtoto wake na kusema sababu zilizopelekea kumtupa mtoto wake ni tatizo la kupatwa na mashetani. Kamanda wa Polisi Kamishna Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja Benedict Mapujila, amesema Mama huyo alikwenda kujisalimisha Kituo Cha Polisi Mahonda na kukiri kuwa yeye ndiye aliyemtupa mtoto huyo kutokana na kupatwa na matatizo ya mashetani ambaye ni mtoto wake Tatu ingawa alimzaa nje ya ndoa. Aidha Kamanda Mapujila, amesema kumtupa mtoto ni Kosa Kisheria hivyo Jeshi la Polisi litamshtaki Mama ili Sheria ifate mkondo wake na kutoa wito kwa jamii kutokufanya maamuzi ambayo yako kinyu...