Skip to main content

“Nimeshiriki michezo tangu nikiwa darasa la tatu kwasasa ni kocha wa timu ya wanawake ya mpira wa miguu maadili yangu ya Kizanzibari yako pale pale” Tamasha Kocha wa timu-Wete Women Club

 Makala Na, Hassan Msellem-Pemba


Mpira wa Miguu au wengi wanapenda kuita Soka, Kandanda, Ndinga au Kabumbu yote yakiwa ni majina sahihi kwa mujibu wa wapenzi wa mchezo huo. Unachezwa uwanjani ukiwa na jumla ya wachezaji 22 kila timu ikiwa na wachezi 11, lengo la mchezo huu ni wachezaji kumiliki mpira kwa kutumia miguu kwa shebaha ya kufunga goli yani kuingiza mpira kwenye wavu zilizosimamishwa kwenye milingoti mitatu yani kulia, kushoto na juu.

Inakadiriwa kuwa mnamo karne ya 21, kulikuwa na wachazaji mpira wapatao milioni 250 kati ya watu bilioni 1.3 Duniani. Mwaka 2010 hadhira ya televisheni ya zaidi bilioni 26 ilitazama mashindano ya kwanza ya kombe ya Soka, fainali za Kombe la Dunia za mwezi wa nne.

Licha umaarufu nakupendwa kwake hakukuwa na timu za wanawake na hii nikutokana na asili ya mchezo huo kuchezwa na wanaume huku baadhi ya mataifa kutokana na Mila na Tamaduni zao wakiami wanawake kushiriki katika mchezo huo ni kwenda kinyume na mil ana tamaduni zao.

Lakini mnamo karne ya 19 timu za mpira wa miguu zikaanzishwa katika mataifa mbali mbali ulimwenguni na hatimae mchezo wa mpira wa miguu kwa wanawake duniani ukawa ni mchezo rasmi kwao na kuweza kushiriki michuano mbali mbali ya kikanda, kitaifa na kimataifa.

Na sasa Dunia kushuhidia wachezaji soka bora wakike kama vile Atiana Bonmati, Sam Kerr na Salma Paralluelo wakiwa mabingwa wa kucheza soka Duniani mwaka 2023/2024, ambapo kwa upande wa Barani Afrika kwa mujibu wa jarida la GOAL mchezaji wat imu ya wanawake ya Tanzania Clara Luvaga anaingia kwenye orodha ya wachezaji soka bara 25 Duniani.

Picha ya Clara Luvaga katikati

Tamasha Ali Omar mwenye umri wa miaka 50, Mkaazi wa Miti Ulaya Wete ni miongoni mwa wanawake ambao michezo iko ndani ya damu yake, kwani alianza kushiriki michezo mbali mbali kama vile mpira wa Kikapu, mpira wavu, urushaji Tufe, riadha nakadhalika tangu akiwa darasa la tatu Skuli ya Miti Ulaya Kisiwani Unguja akiwa wastani wa umri wa miaka 12 mwaka 1974, na kuendeleza kukaza msuli hadi akiwa Sekondari Skuli ya Utaani Wete Pemba ambapo alifanikiwa kushiriki mashindano mbali mbali ya kikanda na kitaifa

Tamasha alisema licha ya wanawake wengi kukumbana na vihunzi kadhaa wanaposhiriki kwenye michezo hususan mpira wa miguu lakini kwake imekuwa ni tofauti kwani alipata baraka zote kutoka kwenye familia yake, walimu wa skuli n ahata jamii iliyokuwa inamzunguka

“Kiupande wangu nashukuru sana kwa kipindi nilipokuwa mdogo sikukumbana na changamoto zozote kwasababu familia yangu ni familia ya michezo kwahivyo sikupata vikwazo kutoka kwa wazazi wangu wala wanajamii na ndio maana nikadumu kwenye michezo kutoka kuwa mchezaji hadi kocha na kuhusu kuwa na tabia mbaya sio kwasababu ya michezo bali khula ya mtu hata asishiriki kwenye michezo” alisema

Tamasha Ali Omar, kocha wa Timu ya mpira ya Wanawake, Wete Women Club.

Kwasasa Tamasha ni mama wa Watoto wanne akiwa na umri wa miaka 50, akiwa kocha wat imu ya mpira wa miguu ya wanawake inayofahamika kwa jina la Wete Women Club, ikiwa na wachezaji 25 na mjumbe wa Soka la Wanawake Zanzibar

Amesema ukosefu wa Kiwanja rasmi cha kufanyia mazoezi, ukata wa fedha pamoja na maneno yasiyofaa kwa wasichana na wanawake wanaoshiriki mchezo Soka ni miongoni mwa changamoto zinazoikabili Timu ya Wete Women Club, hivyo ameiomba Serikali na wadau wa Soka Visiwani Zanzibar kuboresha mazingira ya Wana michezo wanawake Ili waweze kushiriki katika michezo pasi na vikwazo.

"Timu ipo lakini hatuna Uwanja rasmi wa kufanyia mazoezi tunajibanza banza tu kwenye viwanja vya watu pia hatuna uwezo wa kifedha wakutoka nje ya Kisiwa cha Pemba hivyo tunaiomba Serikali na wadau wa michezo watufikirie Ili na Timu za Soka za Wanawake ziweze kushiriki mashindano mbali mbali na kusonga mbele" alisem

Akizungumzia mafanikio aliyoyapata kutokana na michezo alisema amefanikiwa kushiriki mashindano mbali mbali ndani nan je ya Visiwa vya Zanzibar, kujipatia fedha, umaarufu pamoja kuwa na afya imara mithili ya chuma cha pua.

Aisha Haji Ali na Mafunda Hamad Shehe maarufu Nipe wakaazi wa Miti Ulaya Wete ni miongoni mwa wachezaji wa timu ya Wete Women Club, walisema wanamshukuru Bi. Tamasha kuanzisha timu hiyo kwani inawasaidia kwa kiasi kikubwa kuibua, kuendeleza na kuwaisaidia wasichana na wanawake wenye vipaji vya kucheza mpira katika Mkoa wa Kaskazini Pemba hasa Mji wa Wete

Lakini licha kuanzishwa kwa timu hiyo walisema wanakumbana vikwazo mbali mbali vikiwemo vya kurudishwa nyuma ya kushiriki kwenye mchezo huo kwa kisingizio cha kukiuka mila na utamaduni licha kuvaa mavazi ya stara.

Walisema “kwakweli tunamshukuru sana kocha wetu Bi. Tamasha kwa kuanzisha timu ya mpira ya wanawake kwasababu imeweza kutusaidia sana sisi wanasoka wanawake licha ya kwamba tunakumbana na vikwazo mbali mbali kutoka kwa wanajamii lakini hatujali kwavile tunaona faida ya tunachokifanya”

Aisha Haji Ali, mchezaji Timu ya Wete Women Club

Mustafa Hassan Suleiman, ni mume wa Tamasha na Kocha maarufu Visiwani Zanzibar wa Soka Zanzibar alisema tangu afunge ndoa na nguli huyo wa michezo na kocha wat imu ya mpira ya wanawake hajawahi kuona mabadiliko yoyote ya tabia zisizomridhisha na kwamba ameridhia kushiriki kwenye michezo kutokana na faida mbali mbali anazozipata ikiwemo umaarufu, fedha na kuwa afya bora.

“Binafsi tangu nifunge ndoa na Tamasha sijawahi kuona labda amevaa mavazi yanayokwenda kinyume na mila, utamaduni na silka zetu Wazanzibari na sio baada ya kufunga nae ndoa hata kabla ya ndoa kwahivyo nimempa rukhsa na ridhaa kufanya shughuli zake za michezo nak ama unavyojua kuwa ni kocha wa timu ya mpira wa miguu ya wanawake na inafanya vizuri katika mashindano mbali mbali lakini pia tangu niishi na Tamasha sio aghalabu kumsikia anaumwa sijui homa, presha, sukari nakadhalika na ana miaka 50 sasa” alisema

Mwandishi wa Makala haya, alifanikiwa kuzungumza na baadhi ya wananchi na majirani wa Tamasha ambapo wote walithibitisha kuwa kushiriki michezo kwa mama huyo hakujaathiri hata chembe ya Mila na Utamaduni wa maeneo hayo aidha kutokana na mavazi yake au vitendo vyengine vya visivyo vya maadili.

Asha Hussein Omar, ni miongoni mwa majirani wa nguli huyo wa michezo alisema “Mimi tangu kuhamia hapa namfahamu Tamasha kama mwanamke anayependa michezo sana kila siku saa 12 asubuhi na saa 11 jioni anatoka na vijana wanakwenda mazoezi lakini sijawahi kumuona amevaa mavazi yasiyo ya staha au kusikia labda ana tabia mbaya za uhasharati nadhani tabia hizo zinatokana na mtu mwenyewe hata asiwe mwana michezo”

Kuna haja kwa Serikali na wadau wa Michezo Visiwani Zanzibar kufumbua macho upya kuangalia uboreshwaji wa mazingira ya michezo kwa wasichana na wanawake ikiwemo ujengwaji na uboreshwaji wa viwanja, kuandaa makocha, pamoja na kuwepo kwa Sera ya usawa wa Kijinsia kwenye michezo.



Comments

Popular posts from this blog

MWANAMKE AJINYONGA, SABABU WASI WASI - PEMBA

NA, HASSAN MSELLEM - PEMBA PICHA KUTOKA MAKTABA Mwanamke aliyefahamika kwa jina la Raya Darusi Abdallla miaka 48, mkaazi wa Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, amefariki Dunia kwa kidaiwa kujinyonga kutokana na Msongo wa mawazo. Tukio Hilo limetokea Novemba 30.2025 saa 11 alfajiri huko Mbuzini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Omar Salum Ali, ambaye ni shemeji wa marehemu amesema kabla ya marehemu alikuwa na sumbuliwa na Msongo wa mawazo kutokana na kumpoteza kaka yake ambaye alifariki hivi karibuni, kugundulika kuwa ana maradhi ya sukari, mtoto wake wa kiume wa miaka 25, kuwa na ugonjwa akili hali iliyopelekea kupatwa na Msongo wa mawazo na kuamua kujinyonga. Katibu wa Sheha (Katibu wa Mwenyekiti) Shehia ya Mbuzini Yakub Ali Msabah, amesema alipata taarifa za tukio Hilo kutoka kwa Sheha wa Mbuzini kuhusu tukio baada ya kufika eneo la tukio waliukuta mwili wa Mama huyo ukiwa unanin'gia kwenye dari ya Nyumba ambayo alikuwa anaishi zamani. Kutoka tarehe 18 ...

Mariam Muhene – mfano wa kuigwa kwa wanawake kwenye ulingo wa siasa ni

MAKALA NA, HASSAN MSELLEM -PEMBA Tangu Tanzania iruhusu mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, Mariam Muhene alijiunga na chama cha Civic United Front (CUF) ambapo mwaka 1995, aligombea nafasi ubunge wa viti maalumu na kuvuka hatua zote ikiwemo kula kiapo mahkamani lakini hakufanikiwa kukikalia kiti hicho. “Mwaka 1995 niligombea ubunge wa viti maalum na nikapita kila kipengele mtu wa kwanza wilaya, taifa bodi ya uongozi, nikala kiapo mahkmanai lakini katika nafasi mbili zilizoletwa kwa kila mkoa Kusini na Kaskazini Pemba mimi sikubahatika” amesema  Safari yake ya kisiasa za upinzani iliendelea na mnamo mwaka 2000, aligombea nafasi ya ubunge wa kuchahguliwa kupitia chama cha Allience for Democratic Change (ADC) Jimbo la Chake Chake lakini kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwe mawakala wa Chama chake kutokuruhisiwa kuingia kwenye vya kupiga kura jambo ambalo amesema lilichangia kukosa nafasi hiyo. Kwasasa Mariam Mohammed Muhene anashika nafasi ya Kamishna wa ADC kanda ya Pemba, nafas...

WATOTO KUJINYONGA ZANZIBAR, UTAFITI WAHITAJIKA.

HABARI NA, HASSAN MSELLEM, PEMBA Picha kutoka mtandaoni Visa vya watoto kujinyonga vimeanza kuwatia khofu na mashaka wazazi na walezi katika Visiwa vya Unguja na Pemba. Mashaka na khofu hiyo imeibuka baada ya matukio mawili mfululizo ya watoto wawili mmoja akiwa umri wa miaka (5) na mwengine (9) kuripotiwa kufariki dunia kwa kujinyonga kati ya tarehe 7 na 9 mwezi huu wa kumi mwaka 2025 kupitia kipindi cha Mawio kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC kila siku kuanzia saa 12:40 asubuhi. Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 7.10.2025 mwandishi Masanja Mabula aliripoti tukio la Fatma Omar Kidere mwenye umri wa miaka tisa (9) mkaazi wa Mtondoo Jeuri Makaangale Wilaya ya Micheweni Mkao wa Kaskazini Pemba, amekutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa unanin’ginia kwa kutumia mtandio Jirani wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Khamis Ali, amesema amepata taarifa za tukio hilo akiwa kazini baada ya kupigiwa simu na mke wake kumpa taarifa za kutokea kwa tukio hilo na kuondoka kazin...